Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, August 29, 2010


Matumizi endelevu ya kipandio hiki ama dhahama inakurubia...mnijuze waungwana!

Posted by BM. on Sunday, August 29, 2010

Jana katika pitapita yangu ya kununua bidhaa kwa ajili ya Iftar jioni nikakutana na bidhaa zenye majina yaliyonifanya nizinunue.

Futari; inasubiri magharibi tu kuliwa...

Kifuniko cha Juisi ya TBC


Nimekutana na kahawa ya Kilimanjaro na juisi ya TBC ...tamu ladha yake ...lakini ina uhusiano? na...!

Posted by BM. on Sunday, August 29, 2010

Posted by BM. on Sunday, August 29, 2010

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, jana Jumamosi kilizindua kampeni zake katika viwanja vya Jangwani huko Dar ambapo viongozi walinadi Ilani ya chama hicho.

Mgombea uraisi wa chama cha CHADEMA Dr. Wilboard Slaa akihutubia umati wa wafuasi wake Dar jana..

Maelfu ya wakazi wa Dar es salaam waliojitokeza kumsikiliza Dr. Slaa.

Posted by BM. on Saturday, August 28, 2010



Mgombea wa Uraisi Dr.J.Kikwete akiwa katika mikutano ya kuomba ridhaa kwa waajiri wake wa kulitumikia taifa kwa miaka mingine mitano hapa anawasili kijiji cha Buhingwe , Kigoma vijijini ....


Mama mlemavu Jocyceline Paulo akiteta na Dr. J.K katika kijiji cha Rusahunga..(thenksi bratha Mithupu)

Posted by BM. on Saturday, August 28, 2010

Kenya imeandika historia mpya ya utawala nchini humo kwa kuidhinisha katiba mpya, iliyotungwa na wananchi wenyewe, baada ya ile iliyokuwa ikiitumia kabla ya kupata uhuru wake mwaka 1963. Rais Mwai Kibaki, aliwaongoza maelefu ya raia wake walioshuhudia akitia saini katiba mpya ya nchi hiyo katika sherehe zilizofanyika viwanja vya Bustani ya Uhuru mjini Nairobi jana Ijumaa.

Mh. Kibaki akitia saini katiba mpya..

Baada ya kutia saini nakala sita za katiba hiyo, wimbo wa taifa la Kenya ukapigwa na kufuatiwa na mizinga 21 ya heshima. Rais Kibaki, Waziri Mkuu Raila Odinga, Makamu wa Rais Kalonzo Musyoka, Spika wa bunge na wabunge wamekula kiapo cha kuilinda, kuitetea, na kuiheshimu katiba hiyo mpya kwa manufaa na ustawi wa taifa la Kenya na watu wake.Katiba hiyo mpya inabadili namna madaraka yanavyogawanywa na kusimamiwa nchini humo.
Katiba hiyo imepangwa kuzuia aina yoyote ya vurugu kama zile zilizofuatia baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007, wakati zaidi ya watu elfu moja waliuawa kutokana na mgogoro wa kupinga matokeo yaliyompa ushindi Rais Kibaki. Pia ina udhibiti mkubwa kuhusu madaraka ya rais, na inatoa madaraka kwa serikali za majimbo na kuwaongezea uhuru wananchi. Miongoni mwa viongozi wa mataifa ya kigeni waliohudhuria ni Rais Omar Al Bashir wa nchi jirani ya Sudan ambaye anatakiwa na mahakama ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa kivita, kwa tuhuma za kuendesha mauaji ya halaiki katika jimbo la Darfur nchini Sudan.

Alikuwepo..

Akizungumzia wito wa kuitaka Kenya kumkamata Rais huyo wa Sudan, Waziri wa mambo ya nje wa Kenya, Moses Wetangula, amekaririwa akisema, Rais Bashir yupo nchini hapa kwa mwaliko uliofanywa na serikali ya Kenya kwa jirani zake wote kuwaomba kuhudhuria tukio hili la kihistoria., Wetangula amesema, "Huwezi kumdhuru au kumfedhehesha mgeni wako, huu si utaratibu, desturi na maadili ya Kiafrika."
Inaelezwa kuwa hafla ya kuipokea siku hiyo zilifanyika pia katika ofisi zote za balozi za Kenya zilizopo ughaibuni...hebu tuiangalie Tokyo...

SHEREHE ZILIZOFANYIKA TOKYO

Balozi wa Kenya Nchini Japani Mh. Benson Ogutu akiwahutubia waalikwa waliokusanyika katika Ubalozi wao hapa Tokyo. Ilikuwa hotuba ya kuelezea kule Kenya ilikotoka , ilipo na matarajio yao. Kulikuwa na kunywa , kula na kubadilishana maoni...fuatilia kwa njia ya picha.


Waalikwa katika hafla ya Tokyo...

Uwakilishi ulikuwepo...strong>

Wadau muhimu..strong>


Tupo na mmoja wa washiriki wa hafla hii ni mkongwe wa fani ya utangazaji kutoka Kenya Bw. Ally Attasi mwenye shati jeusi. Huyu aliwahi kuitangazia KBC miaka ya nyuma na baadaye akaifanyia kazi NHK-Japani . Hivi sasa anaishi hapa Japani akifanya shughuli zake binafsi...Take 5 Bro.

Picha ya kumbukumbu; Na Mh. Balozi wa Kenya hapa Japani Mh. Benson Ogutu .(katikati)Pamoja naye ni Mie na Mtangazaji mwenzangu wa Redio Japani-NHK, Edward Kadilo ambaye pia ni mwajiriwa wa KBC.


Mmoja wa wadau wa NHK Bi. Maureen Waweru naye alikuwepo katika hafla hiyo; hapa ni kwenye ushoroba wa Ubalozi wa Kenya hapa JP

Posted by BM. on Tuesday, August 24, 2010


Ankal Bahati Makunzo akiwa Joberg , Afrika Kusini...Take 5...uncle imetulia..

Posted by BM. on Tuesday, August 24, 2010


Vazi linapendekezwa litumiwe na watembea kwa miguu ili kuepusha ajali. ...Nafikiria tu likivaliwa na watui jijini Dar es salaam , na mtu akakosea na kubofya kushoto kumbe anakwenda kulia si balaa...watu bwana!

Posted by BM. on Tuesday, August 24, 2010


Kufunga na kusoma kitabu kitakatifu ..Quraan!

Posted by BM. on Tuesday, August 24, 2010


Picha ya kumbukumbu ...Mh. Jakaya Kikwete na Mkurugenzi wa kampuni moja ya uuzaji magari iliyo na makao yake nchini Japanib Jumbe Bagilo walipokutana , wakati JK alipofanya ziara hapa Japani....

Posted by BM. on Tuesday, August 24, 2010

Joto limeshika kasi nchini Japani hususan jiji la Tokyo. Jua kali , joto jingi. Liliwahi kufika 39 hapa Tokyo na jana likashuka na kufikia 33.6C Hata hivyo halikutuzuia kutoka mtaani. Baada ya kazi za ofisini tuliingia katika mitaa ya Harajuku kuona pilikapilika za wakati wa joto...

Mtaa maarufu wa Harajuku unavyoonekana ..

Mwenzetu Edward Kadilo alijichanganya na vijana wa Kijapani katika mtaa wa sikukuu...
Pozi la picha (Kutoka Kushoto) Specioza -Mama J, Ana Kwambaza , na Mie...

Posted by BM. on Friday, August 20, 2010


Wachambuzi wa mambo mnapata ujumbe gani hapo...bila shaka upo!

Posted by BM. on Thursday, August 19, 2010


Dr. JK


Mwl. J.K

Posted by BM. on Thursday, August 19, 2010


Mbunge wa kuteuliwa anayemaliza muda wake anayewakilisha maalbino, Mh. Al Shaimaa John Kwegyir akiteta jambo na Rais Jakaya Kikwete wakati wa hafla ya kuzindua nakuichangia taasisi ya Goodhope Star Foundation ambayo itatetea na kutoa huduma kwa maalbino..

A court in Tanzania has sentenced a Kenyan accused of trying to sell an albino to 17 years in jail and a fine of more than $50,000 (£41,200).
The court sentenced Nathan Mutei after he pleaded guilty to human trafficking.
Police said they arrested Mutei in a sting operation as he tried to sell an albino fellow Kenyan for the equivalent of more than $250,000.
Albino body parts are prized in parts of Africa, with witch-doctors claiming they have special powers. The albino, Robinson Mkwama, is being escorted home to Kenya with a police guard, the BBC's Eric Nampesya reports from Tanzania.
Mutei, 28, was arrested just outside the town of Mwanza. In the sting operation, which was announced on Tuesday, police pretended to be businessmen buying albino body parts.


The regional police commander, Simon Siro, told the BBC that Mr Mutei had tricked Mr Mkwama, 20, into believing he would secure a job in Tanzania as a lorry driver's assistant.In Tanzania, the body parts of people living with albinism are used by witch-doctors for potions which they tell clients will help make them rich or healthy.Dozens of albinos have been killed, and the killings have spread to neighbouring Burundi.Tanzanian authorities have promised to crack down on albino traffickers, and several people have been sentenced to death in connection with killings.
Source;BBC website

Posted by BM. on Thursday, August 19, 2010

Mwimbaji wa kundi moja la muziki nchini Ujerumani lijulikanalo kama No Angels, amekiri kosa la kufanya mapenzi bila kinga na wanaume kadhaa bila kuwaonya kuwa ana virusi vya HIV.


Mwanamuziki huyo Nadja Binaissa mwenye umri wa miaka 28, alikuwa akizungumza katika ufunguzi wa kesi yake katika mji wa Darmstadt nchini Ujerumani.
"Ninaomba sana radhi", Bi. Benaissa ameiambia mahakama. Hata hivyo amekanusha kuambukiza mtu yeyote kwa makusudi.
Anakabiliwa na mashitaka ya kudhuru mwili kwa kutuhumiwa kumuambukiza mtu mmoja virusi.
Aidha, ameshitakiwa kwa tuhuma za kutaka kudhuru mwili wa mtu kwa kutuhumiwa kufanya mpenzi na wanaume wawili ambao hata hivyo hawakuambukizwa.
Iwapo atakutwa na hatia, Bi. Benaissa huenda akakabiliwa na kifungo cha kati ya miezi sita hadi miaka 10.
Baada ya kesi kufunguliwa, shirika la habari la Ujerumani DAPD liliandika taarifa kutoka kwa mwanasheria wa Bi. Benaissa, ikisema mwanamuziki huyo hakuweza kushughulikia vyema suala la kuishi na virusi vya HIV, na pia kukiri kufanya mapenzi bila kutumia kinga.
Lakini mwimbaji huyo alisema: " Hata mara moja sikutaka mpenzi wangu kuambukizwa."
Bi. Benaissa alikamatwa mjini Frankfurt mwaka jana, muda mfupi kabla ya kufanya onyesho lake la muziki, na aliwekwa rumande kwa siku 10.


Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI wameshutumu mamlaka za huko kwa jinsi walivyolishughulikia suala la kukamatwa kwa msanii huyo, na kuonya dhidi ya kuharakisha suala la uhalifu wa maambukizi ya virusi vya HIV.

Kwa mujibu wa waendesha mashitaka, Bi. Benaissa alijijua kuwa na virusi vya HIV tangu mwaka 1999.
Mpenzi wake wa zamani, ambaye ana virusi vya HIV, anasema mwimbaji huyo alimuambukiza mwaka 2004, na anatazamiwa kufika mahakamani mjini Darmstadt kama mlalamikaji.
Mwezi Novemba mwaka jana, Bi. Benaissa katika tamasha la UKIMWI mjini Berlin, alijitokeza na kusema hadharani : "Jina langu ni Nadja Benaissa, nina miaka 27, nina mtoto wa kike na ninaishi na virusi vya HIV."


Kundi la waimbaji la No Angels liliundwa mwaka 2000 katika kipindi cha televisheni cha waimbaji wa kimataifa, na baadaye kurekodi vibao vilivyovuma na hatimaye kuwa kundi la kina dada lenye mafanikio zaidi nchini humo.
Mwaka 2007, waimbaji hao waliungana tena na kushiriki katika mshindano ya wimbo bora wa Eurovision, na kushika nafasi ya 23.
Kesi ya Bi. Benaissa inatarajiwa kumalizika mwisho wa mwezi huu.

Posted by BM. on Thursday, August 19, 2010

Mwanamke mwenye matiti makubwa kuliko wanawake wote duniani ametakiwa achague moja matiti hayo yaondolewe ili aweze kuishi au la afariki akiwa na rekodi yake ya matiti makubwa kuliko wanawake wote duniani.


Sheyla Hershey alipata maambukizi kwenye matiti yake wakati akifanyiwa operesheni ya kuyaongeza matiti yake ambayo yana ukubwa wa 38KKK.Mrembo huyo wa Brazili mwenye umri wa miaka 30 aliambiwa na madaktari kuwa kuna uwezekano wa asilimia 80 ataweza kuliokoa titi lake moja. Lakini mrembo huyo amesema kuwa ni bora matiti yote yaondolewe kuliko abaki na titi moja.
"Uwezekano wa kuyaokoa matiti yake yote mawili ni mdogo sana kati ya asilimia 10 na 20", alisema Sheyla.Sheyla alikuwa anafanyiwa operesheni nchini Marekani ili kurekebisha matiti yake ambayo yalipata maambukizi alipofanyiwa operesheni nchini Brazili mwaka jana.Hiyo ilikuwa operesheni yake ya 10 ya kurekebisha matiti yake tangu alipojifungua mtoto mwaka jana.Madaktari wa Marekani walikataa kuongeza ukubwa wa matiti yake kwakuwa ni marufuku nchini Marekani kuweka zaidi ya lita 4.5 za silicone kwenye matiti.Maambukizi aliyopata yalisababisha apate tabu kupumua.
"Niko kwenye maumivu makali ambayo najaribu kuyapunguza kwa kunywa madawa, maambukizi niliyopata ni sawa sawa na kansa", alisema Sheyla.

"Njia pekee ya kuondokana na maumivu haya ni kuyaondoa matiti haya", alisema Sheyla ambaye alikuwa akijivunia sana rekodi yake ya kuwa mwanamke mwenye matiti makubwa kuliko wanawake wote duniani.

Posted by BM. on Sunday, August 15, 2010

Halmashauri kuu ya CCM-NEC imetangaza majina ya wagombea ubunge kupitia chama hicho kwa mikoa 13. Kwa mujibu wa ORODHA KAMILI


WALIOTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI KATIKA UCHAGUZI MKUU 2010

1.MKOA WA KIGOMA
(i) Mjini: Peter Serukamba,
(ii)Kigoma South: Gulam Hussein Shaaban Kifu,
(iii)Kasulu Urban: Neka Raphael Neka,
(iv)Kasulu Rural: Daniel Nsanzugwanko,
(v)Manyovu: Albert F. Ntabaliba,
(vi)Buyungu: Christopher Chiza,
(vii)Muhambwe: Jamal Abdallah Tamimu,
(viii)Kigoma North: Rabinson, F. Lembo.

2.MKOA WA KILIMANJARO
(I) Moshi Mjini:Justin Salakana,
(ii) Moshi Vijijini: Dk. Cyril Agust Chami,
(iii)Rombo: Basil Pesambili Mramba,
(iv)Same Mashariki): Anne Kilango Malecela,
(v)Same Magharibi: Dk. David Mathayo David,
(vi)Hai: Fuya Godwin Kimbita,
(vii) Vunjo: Chrispin Theobald Meela,
(viii) Mwanga: Profesa Jumanne Maghembe,
(ix)Siha, Aggrey D.J. Mwanri.

3.MKOA WA MANYARA:
(i)Babati mjin:Kisyeri Werema Chambiri,
(ii)Babati Vijini: Jitu Vrajil Soni,
(iii)Hanang: Dk. Mary Michael Nagu,
(iv)Kiteto: Benedict Ole Nangoro
(v) Mbulu:Philip Sang’ake Marmo,
(vi)Simanjiro:Christopher Ole Sendeka.

4.MKOA WA MARA

(i) Musoma mjini: Vedasto Manyinyi,
(ii)Musoma vijijini:Nimrod Elirehema Mkono,
(iii)Mwibara: Alphaxard Kangi Lugola,
(iv)Bunda: Stephen Masatu Wasira,
(v)Rorya: Lameck Okambo Airo,
(vi)Tarime, Nyambari Chacha Nyangwine,
(vii)Serengeti: Dk. Stephene Kebwe Kebwe.

5.MKOA WA MBEYA
(i) Mbeya Mjini: Benson Mwailugula Mpesya,
(ii) Mbeya Vijijini: Luckson Ndage Mwanjala,
(iii) Kyela: Dk Harrison George Mwakyembe,
(iv)Mbarali: Dickson Modestus Kilufi,
(v)Lupa: Victor Kilasile Mwambalaswa,
(vi) Songwe:Philipo Augustino Mulugo,
(vii) Rungwe Mashariki: Profesa Mark James Mwandosya,
(viii) Rungwe Magharibi: Profesa David Homeli Mwakyusa,
(ix) Ileje: Aliko Nikusuma Kibona,
(x)Mbozi Mashariki: Godfrey Weston Zambi,
(xi)Mbozi Magharibi: Dk. Luka Jelasa Siame.


6. MKOA WA MOROGORO
(i)Morogoro Mjini:Aziz Mohamed Abood,
(ii)Morogoro Kaskazini: Dk. Lucy Sawera Nkya,
(iii)Morogoro Kusini: Innocent Kalogeris,
(iv)Mvomero: Amos Gabriel Makala
(v) Ulanga Mashariki: Celina Ompeshi Kombani,
(vi)Ulanga Magharibi: Haji Hussein Mponda,
(vii)Gairo: Ahmed Mubukhut Shabiby
(viii)Kilosa, Mustafa Heidi Mkulo,
(ix)Mikumi: Abdulsalaam Suleiman,
(x)Kilombero: Abdul Rajab Mteketa.

7.MKOA WA TABORA
(i)Urambo Mashariki: Samwel John Sitta
(ii)Urambo Magahribi: Juma Athuman Kapuya,
(iii)Tabora Mjini: Ismail Aden Rage,
(iv)Igunga: Rostam Abdulsasu Aziz,
(v)Sikonge: Said Juma Nkumba
(vi) Igagula: Athuman Rashid Mfutakamba
(vii) Tabora: Sumar Shaffin Mamlo,
(viii)Bukene: Seleman Jumanne Zedi
(ix)Nzega:Dr. Hamisi Andrea Kigwangala

8.MKOA WA TANGA
(i)Tanga mjini: Omari Rashid Nundu
(ii)Kilindi: Beatrice Matumbo Shelukind
(iii)Muheza: Herbert James Mntangi
(iv)Mkinga: Danstan Luka Kitandula
(v)Pangani: Salehe Ahmed Pamba
(vi)Lushoto: Henry Daffa Shekifu
(vii)Bumbuli: January Makamba
(viii)Korogwe Mjini:Yusuph Nasri
(ix)Mlalo:Brig. Gen. Hassan Athuman Ngwilizi
(x)Korogwe Vijijini: Stephen Ngonyani
(xi)Handeni: Dr. Abdalah Omari Kigoda

10.MKOA WA DAR ES SALAAM
(i).Kinondoni: Idd Mohamed AZAN
(ii).Ubungo: Hawa Mgonja NG’UMBI
(iii).Kawe: Angella Charles KIZIGHA
(iv).Ilala: Musa Azan ZUNGU
(v).Ukonga: Eugen Elishirima MWAIPOSA
(vi).Segerea:Dr. Milton Makongoro MAHANGA
(vii).Temeke: Abbas Zuber MTEMVU
(viii).Kigamboni:Dr. Faustine NDUGULILE

11.MKOA WA LINDI
(i)Lindi Mjini:Ndugu Mohamed ABDULAZIZ
(ii)Mtama:Ndugu Bernard Kamillius MEMBE
(iii)Mchinga:Ndugu Said M. MTANDA
(iv)Nachingwea:Ndugu Mathias Meinrad CHIKAWE
(v)Ruangwa:Ndugu Kassim MAJALIWA
(vi)Kilwa kaskazini:Ndugu Murtaza Ali MANGUNGU
(vii)Kilwa Kusini:Ndugu Ramadhan Rashid MADABIDA
(viii)Liwale:Ndugu Faith Mohamed MITAMBO

12.MKOA WA PWANI
(i)Bagamoyo: Dr. Shukuru J. Kawambwa
(ii)Chalinze: Saidi Athuman Bwanamdogo
(iii)Kisarawe: Seleman Saidi Jafo
(iv)Kibiti: Abdul J. Marombwa
(v)Kibaha Vijijini: Mahamud Abuu Jumaa
(vi)Kibaha Mjini: Silvestery F. Koka
(vii)Mkuranga: Adam Kighoma Malima
(viii)Rufiji: Dr. Seif Seleman Rashid
(ix)Mafia: Abdulkarim E. Shaha

13.MKOA WA RUKWA
(i)Kwela: Malocha Aloyce Ignace
(ii)Kalambo: Kandege Sinkamba Josephat
(iii)Nkasi Kaskazini: Ally Mohamed Kessy
(iv)Nkasi Kusini:Deusderius Mipata
(v)Mlele: Mizengo Kayanza Peter Pinda
(vi)Mpanda Kati (mjini): Sebastian Simon Kapufi
(vii)Sumbawanga Mjini: Aeshi Khalfan Hilaly
(viii)Mpanda Vijijini: Moshi S. Kakoso

14.MKOA WA SHINYANGA
(i)Shinyanga Mjini: Steven Julius Masele
(ii)Kishapu: Nchambi Seleman Masoud
(iii)Kahama: James Daud Lembeli
(iv)Msalala: Maige Ezekiel Magolyo
(v)Solwa: AhmeD Ally Salum
(vi)Bukombe: Emanuel Jumanne Luhahula
(vii)Mbogwe: Masele Agustino Manyanda
(viii)Bariadi Mashariki: Makondo Martine Kaunda
(ix)Bariadi Magharibi: Chenge Andrew John
(x)Maswa Mashariki: Bunyongoli Peter Edward
(xi)Maswa Magharibi: Kisena Robert Simon
(xii)Meatu:Salum Khamis Salum
(xiii)Kisesa: Joelson Luhaga Mpina.

15.MKOA WA SINGINDA
(i)Singida Mjini:Mohamed Gulam Dewji
(ii) Manyoni Mashariki:Capt.(mstaafu) John Chiligati
(iii)Manyoni Magharibi: John Paul Lwanji
(v)Iramba Magharibi: Mwigulu Lameck Nchemba Matelu
(vi)Iramba Mashariki:Salome David Mwambu
(vii)Singida Kaskazini:Lazaro Samwel Nyalandu
(viii)Singida Magharibi:Alhaj Mohamed Misanga
(ix)Singida Mashariki:Jonathan Andrew Njau

16.MKOA WA ARUSHA
(i)Arusha:Dr. Batilda BURIANI
(ii)Arumeru Mashariki: Jeremiah Solomon SUMARI
(iii)Arumeru Magharibi: Goodluck Joseph Ole MEDEYE
(iv)Karatu: Dr. Wilbald Slaa LORRI
(v)Longido: Michael Lekule LAIZER
(vi)Monduli: Edward Ngoyai LOWASSA
(vii)Ngorongoro: Saning’o Kaika Ole TELELE

17.MKOA WA IRINGA
(i)Iringa Mjini: Monica Ngenzi MBEGA
(ii)Isimani: William Vangimembe LUKUVI
(iii)Kalenga: William Augustino MGIMWA
(iv)Kilolo:Prof. Peter Mahamudu MSOLLA
(v)Ludewa: Deo Haule FILIKUNJOMBE
(vi)Makete:Dr. Binilith Satano MAHENGE
(vii)Mufindi Kaskazini: Mohamed Hassan MGIMWA
(viii)Mufindi Kusini: Menrad Lutengano KIGOLA
(ix)Njombe Kaskazini:Deo Kasenyenda SANGA (Jah People)
(x)Njombe Kusini: Anne Semamba MAKINDA
(xi)Njombe Magharibi: Gerson Hosea LWENGE

18.MKOA WA KAGERA

(i)Nkenge: Assumpter Nshunju MSHAMA
(ii)Bukoba Mjini: Khamis S. KAGASHEKI
(iii)Bukoba Vijijini:Ndugu Jasson S. RWEIKIZA
(iv)Muleba Kaskazini: Charles J. MWIJAGE
(v)Muleba Kusini: Anna K. TIBAIJUKA
(vi)Chato: John Pombe MAGUFULI
(vii)Kyerwa: Eustace O. KATAGIRA
(viii)Karagwe: Gosbert B. BLANDES
(ix)Biharamulo: Oscar R. MUKASA
(x)Ngara: Deogratias Aloys NTUKAMAZINA

****************************************

WALIOTEULIWA KUGOMBEA UBUNGE KATIKA BUNGE LA JAMHURI YAMUUNGANO WA TANZANIA KWA KUPITIA CHAMA CHA MAPINDUZI (ZANZIBAR)
19.MKOA WA KASKAZINI PEMBA
i.Jimbo la Konde:Salum Nafoo *OMAR
ii.Jimbo la Mgongoni: Mselem Rashid MSELEM
iii.Jimbo la Micheweni: Khamis Juma OMAR
iv.Jimbo la Tumbe: Rashid Abdalla KHAMIS
v.Jimbo la Wete:Ali Rashid ALI
vi.Jimbo la Mtambwe:Khamis Seif ALI
vii.Jimbo la Kojani:Hafidh Said MOH’D
viii.Jimbo la Ole: Masoud Ali MOH’D
ix.Jimbo la Gando: Haji Faki JUMA

23.MKOA WA KASKAZINI UNGUJA
i.Jimbo la Chaani:Ali Juma HAJI (Chepe)
ii.Jimbo la Matemwe:Kheir Khatib AMEIR
iii.Jimbo la Mkwajuni: Jaddy simai JADDY
iv.imbo la Nungwi: Ame Pandu AME
v.Jimbo la Tumbatu: Juma Othman ALI
vi.Jimbo la Bumbwini: Ramadhan Haji SALEH
vii.Jimbo la Donge Sadifa Juma KHAMIS
viii.Jimbo la Kitope:Balozi Seif Ali IDDI

24.MKOA WA KUSINI PEMBA
i.Jimbo la Chake Chake: Hamad Bakar ALI
ii.Jimbo la Chonga: Issa Ali JUMA
iii.Jimbo la Wawi: Daudi Khamis JUMA
iv.Jimbo la Ziwani: Juma Ali JUMA
v.Jimbo la Mkoani: Issa Moh’d SALUM
vi.Jimbo la Mkanyageni:Prof.Makame Mnyaa MBARAWA
vii.Jimbo la Chambani: NduguMoh’d Abrahman MWINYI
viii.Jimbo la Mtambile: NduguYakoub Moh’d SHOKA
ix.Jimboa la Kiwani:Ndugu Rashid Abdalla RASHID

25.MKOA WA KUSINI UNGUJA
i.Jimbo la Makunduchi: Samia Suluhu HASSANI
ii.Jimbo la Muyuni: Mahadhi Juma MAALIM
iii.Jimbo la Koani:*Ndugu Amina Andrew *CLEMENT*
iv.Jimbo la Uzini: Moh’d Seif KHATIB
v.Jimbo la Chwaka: Yahya Kassim ISSA

26.MKOA WA MJINI MAGHARIBI
i.Jimbo la Mtoni: Ussi Ame PANDU
ii.Jimbo la Mfenesini: Nasib Suleiman OMAR
iii.Kiembesamaki: Waride Bakari JABU
iv.Jimbo la Dole:Sylvester Massele MABUMBA
v.Jimbo la Magogoni: Issa Abeid MUSSA
vi.Jimbo la Bububu:Juma Sururu JUMA
vii.Jimbo la Dimani: Abdalla Sheria AME
viii.Mwanakwerekwe: HajiJuma SEREWEJI
ix.Jimbo la Fuoni:Said Mussa ZUBEIR
x.Jimbo la Chumbuni: Perera Ame SILIMA
xi.Jimbo la Kwahani:Dr.Hussein Ali MWINYI
xii.Jimbo la Mpendae: Salum Hassan Abdalla TURKEY
xiii.Mji Mkongwe: Nassor Juma MUGHEIRY
xiv.Jimbo la Magomeni: Moh’dAmour CHOMBO
xv.Jimbo la Kikwajuni: Hamad Yussuf MASAUNI
xvi.Kwamtipura:Kheir Ali KHAMIS
xvii.Jimbo la Amani: Mussa Hassan MUSSA
xviii.Jimbo la Rahaleo: AbdallaJuma ABDALLA
xix.Jimbo la Jang’ombe: HusseinMussa MZEE

******************************************************

WANACCM/UWT WALIOTEULIWA NAFASI (100) ZA UBUNGE VITI MAALUM WANAWAKE KATIKABUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 2010*

i.Viongozi Wakuu wa UWT
1.Sophia Mnyambi Simba (Mwenyekiti)
2.Amina Nassoro Makilagi (Katibu Mkuu)

Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (Walioshika namba ya Kwanza)

MARA
3.Gaudentia Mugosi Kabaka

TANGA
4.Ummy Ally Mwalimu

MTWARA
5.Agness Elias Hokororo

MANYARA
6.Martha Jachi Umbulla

SHNYANGA
7.Lucy Thomas Mayenga

KUSINI PEMBA
8.Faida Mohamed Bakari

DODOMA
9.Felista Alois Bura

KASKAZINI UNGUJA
10.Kidawa Hamid Saleh

RUVUMA
11.Stella Martine Manyanya

MWANZA
12. Maria Ibeshi Hewa

MBEYA
13. Hilda Cynthia Ngoye

KIGOMA
14.Josephine Johnson Genzabuke

SIMIYU
15.Esther Lukago Midimu

KASKAZINI PEMBA
16.Maida Hamad Abdalla

KUSINI UNGUJA
17. Asha Mshimba Jecha

DAR ES SALAAM
18. Zarina Shamte Madabida

ARUSHA
19.Namalok Edward Sokoinei

TABORA
20. Munde Tambwe Abdallah

KAGERA
21.Benardetha Kasabago Mushashu

GEITA
22.Vick P. Kamata

NJOMBE
23.Pindi Hazara Chana

LINDI
24. Fatuma Abdallah Mikidadi

MOROGORO
25.Getrude Rwakatare

KILIMANJARO
26.Betty E. Machangu

SINGIDA
27.Diana Mkumbo Chilolo

MJINI MAGHARIBI
28. Fakharia Shomari Khamis

PWANI
29. Zaynabu Matitu Vulu

RUKWA
30.Abia Muhama Nyabakari

KATAVI
31.Pudenciana Kikwembe

IRINGA
32.Lediana Mafuru Mng’ong’0

iii.Kundi la Vijana T/Bara (nafasi 4)

33. Sarah Msafiri Ally
34. Catherine V. Magige
35. Ester Amos Bulaya
36. Neema Mgaya Hamid


iv.Kundi la Vijana T/ Zanzibar (Nafasi 2)
37. Tauhida Galos Cassian
38. Asha Mohamed Omar

v.Kundi la NGO’s (Nafasi 2)
39.Rita Louis Mlaki
40.Anna Margreth Abdallah

vi.Kundi la Vyuo Vikuu (Nafasi 2)
41. Dkt. Fenella E. Mukangara
42. Terezya Lwoga Huvisa

vii.Wanawake wenye Ulemavu (Nafasi 2)
43. Ndg. Al-Shaymaa Kwegir
44.Margreth Mkanga

Viii.Kundi la Wafanyakazi (nafasi 2)
45. Angellah Jasmin Kairuki
46.Zainab Rashid Kawawa


ix.Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (walioshika namba ya pili)

KUSINI PEMBA
47. Mwanakhamis Kassim Said

LINDI
48.Riziki Said Lulida

RUVUMA
49.Devotha Mkuwa Likokola

MOROGORO
50.Christina Ishengoma

DODOMA
51.Mariam Salum Mfaki

TABORA
52. Margreth Simwanza Sitta

PWANI
53. Subira Khamis Mgalu

IRINGA
54.Rita E. Kabati

SINGIDA
55.Martha Moses Mlata

KASKAZINI PEMBA
56. Dkt. Maua Abeid Daftari

KAGERA
57. Elizabeth Nkunda Batenga

SHINYANGA
58. Azza Hillal Hamad

KASKAZINI UNGUJA
59. Bahati Ali Abeid

MBEYA
60. Mary Machuche Mwanjelwa

GEITA
61. Josephine T. Chengula

KUSINI UNGUJA
62. Kiumbwa Makame Mbaraka

RUKWA
63. Roweete Faustine Kasikila

MTWARA
64. Anastazia Wambura


TANGA
65. Mary Pius Chatanda

MARA
66.Rosemary Kasimbi Kiligini

DAR ES SALAAM
67. Mariam Nassor Kisangi

MWANZA
68. Kemilembe Julius Lwota

MJINI MAGHARIBI
69. Asha Abdalla Juma

KATAVI
70.Anna Richard Lupembe

SIMIYU
71.Tinner Andrew Chenge

NJOMBE
72. Rosemary Staki Senyamule

KILIMANJARO
73. Shally Josepha Raymond

ARUSHA
74.Halima Mohamed Mamuya

MANYARA
75. Dora Heriel Mushi

KIGOMA
76. Amina Butoye Kanyogoto


x.Kundi la Vijana – TanzaniaBara (nafasi 3)
77. Happyness Elias Lungiko
78. Kasilda Jeremia Mgeni
79. Mboni Mohamed Mhita


xi.Kundi la Vijana – T/Zanziar(nafasi 1)
80. Rabia Abdallah Hamid

xii.Kundi la Vyuo Vikuu (nafasi 1)
81.Rukia S. Mselem

xiii.Kundi la Walemavu (nafasi 1)
82.Hidaya Mjaka Ali

xiv.Kundi la Kapu – (nafasi 18)
83. Janeth Maurice Masaburi
84.Sifa Amani Swai
85.Mwaka Abdurahamani Ramadhani
86.Moshi Kondo Kinyogoli
87.Janath Mussa Kayanda
88.Zulfa Abdalla Said
89.Asha Ramadhani Baraka
90.Aziza Sleyum Ally
91. Mwantum Haji
92. Esther Kabadi Nyawazwa
93.Fatuma Hassan Toufiq
94.Raia Amour Othman
95.Florence E. Kyendesya
96.Aisha Matembe
97.Fatuma Hamza Mohamed
98.Rukia Masasi
99.Nemburis Kimbele
100.Raya Talib Ali

Posted by BM. on Saturday, August 14, 2010

Maveterani watatu wa vita kutoka nchini Marekani wakiwa na ulemavu wa viungo, kila mmoja akiwa na mguu mmoja ulio mzima na mwingine akiwa na miwili yote ya bandia wamefanikiwa kufika kileleni katika mlima Kilimanjaro, Mlima ulio mrefu kuliko wote barani Afrika.


Neil Duncan, 26, alipoteza miguu yake yote kutokana na bomu lililotegwa kando ya barabara huko Afghanistan mwaka 2005;
Maveterani hao wa vita , walishiriki katika vita nchini Vietnam, Afghanistan na Iraq walifika kilele cha mlima huo takriban mita 5,891 juu ya usawa wa bahari sawa na futi (19,330ft). Walitumia siku sita na kudhihirisha kuwa ulemavu sio kutoweza kila.
Wapandaji hao wa mlima walikuwa Dan Nevins, mwenye miaka 37, aliyepoteza miguu yake yote nchini Iraq;
Neil Duncan, 26, alipoteza miguu kutokana na bomu lililotegwa kando ya barabara huko Afghanistan mwaka 2005; na Kirk Bauer, mwenye umri wa miaka 62, alipoteza mguu mmoja katika vita vya Vietnam mwaka 1969.
Dan Nevins,(37)Duncan,( 26), Kirk Bauer(62)
Walipofika Kwenye kituo cha Gillman wakielekea kileleni walionekana na majeraha madogomadogo katika mapaja lakini wakiwa na furaha tele..

Posted by BM. on Saturday, August 14, 2010

Mafuriko yametikisa Kaskazini Magharibi mwa Pakistan na kuleta taharuki kubwa ...wananchi wako katika wakati mgumu.

Hali inapokuwa tete makazi yanahamia katika kiwanja kama hiki...Mkazi wa kijiji cha Shah Jamal

Mitaa ya Pakistan....adha ya mafuriko.

Du sijui nianzie wapi!

Posted by BM. on Friday, August 13, 2010



Viatu vya mkubwa

Posted by BM. on Friday, August 13, 2010


L-R) Isah Luyima, Mugisha Muhamood, Haruna Luyima and Edrisa Nsubuga who are being held as suspects in 11 July twin bombings in Kampala, 12 Aug 2010.

Investigators in Uganda say they have arrested the masterminds behind the twin bomb attacks last month that killed 76 people in Kampala. The four Ugandan men admitted their involvement in the attacks during a news conference Thursday. The bombings targeted a restaurant and a club where people had gathered to watch the World Cup football final. The leader of the attackers said he wanted to kill Americans out of religious conviction. He said he was a member of al-Shabab, the AL-Qaida linked militant group which claimed responsibility for the double suicide blasts. Authorities in Uganda and Kenya have already detained a number of other people they believe were connected to the bombings.


Late last month, a Ugandan court charged three people after arresting about 20 others in connection with the attacks.
Somali militant group al-Shabab had never mounted a major terrorist attack outside Somalia.

Posted by BM. on Friday, August 13, 2010


Zahiri Ally Zorro na Banana Z.A.Zorro..

Posted by BM. on Friday, August 13, 2010


Prof Nangoli (left) seated with the former Tanzanian President Mwalimu Julius Nyerere.

Mwalimu Julius Nyerere , enzi ya uhai wake alipokutana na Raisi wa zamani wa Cuba Fidel Castro...

Posted by BM. on Friday, August 13, 2010


Raisi jakaya Kikwete akishiriki katika ibada...

Posted by BM. on Wednesday, August 11, 2010

Waislamu kote duniani leo wameanza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan huku wengine wakitarajiwa kuanza kufunga kesho alhamisi.Waislamu wanauanza mwezi wa tisa wa kalenda ya kiislamu ambao hujulikana zaidi kama mwezi wa Ramadhan kwa kujizuia kula na kunywa kuanzia alfajiri jua linapochomoza hadi jioni jua linapozama.



Kufunga ni mojawapo ya nguzo tano za Uislamu.Kuanza na kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan hutegemea na kuandama kwa mwezi lakini kumekuwa na mgongano juu ya njia za kugundua kuandama kwa mwezi. Baadhi ya nchi hutaka mwezi lazima uonekane kwa macho na hukataa kutambua kuandama kwa mwezi kwa kutumia njia za kisayansi.
Nchini Saudi Arabia, televisheni ya taifa ya Al-Ekhbariyah ilitangaza kuwa baraza linalohusika na kuthibitisha kuandama kwa mwezi limetoa taarifa kuwa jumatano ndio mwanzo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.Nchi za Qatar, UAE, Bahrain, Kuwait, Misri, Syria, Lebanon, Yemen nazo zimetangaza kuwa mwezi wa Ramadhan unaanza leo jumatano.
Baraza la Waislamu la Jordan lilitangaza kuwa mwezi haujaonekana nchini humo lakini kwakuwa umeonekana nchi za jirani basi na wao wataanza kufunga leo jumatano.
Hata hivyo nchi ya Oman imetangaza kuwa wao wataanza kufunga alhamisi kwakuwa hawajauona mwezi nchini humo.

MIRINDIMO inawatakia waislamu wote duniani mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Posted by BM. on Tuesday, August 10, 2010

Raisi wa Rwanda Paul Kagame ameshinda kwa asilimia 96 katika kura zilizohesabiwa awali ambazo nyingi ni kutoka nje ya nchi hiyo na karibu theluthi moja ya majimbo nchini humo , jambo ambalo dhahiri limempa ushindi....Bado zoezi la kuhesabu kura linaendelea lakini ni katika kuweka kumbukumbu sawa
Unaweza pia kufuatilia umaarufu wa Raisi Kagame kwa kufuatilia ripoti hii ya shirika la habari la Uingereza The Reuters.
object width="640" height="385">

Weye una maoni gani juu ya ushindi huu wa Kagame?

Posted by BM. on Tuesday, August 10, 2010



Indian coast guard vessels and helicopters worked Monday to contain oil spilling from a stricken container ship that collided with another vessel in the Arabian Sea, India's defense ministry said.The Panamanian-registered MSC Chitra smashed into the St. Kitts-registered MV-Khalijia-II on Saturday near Mumbai's Jawahar Lal Nehru port. The accident caused the MSC Chitra to run aground and list heavily, ministry spokesman Capt. Manohar Nambiar told The Associated Press.



Helicopters sprayed chemicals on the oil spill to prevent it from spreading, Nambiar said.The amount of oil leaked was unclear. The environment minister of Maharashtra state told reporters Monday about 2 tons of oil was pouring into the water every hour.The MSC Chitra was carrying several thousand tons of oil products such as diesel and lubricants, Environment Minister Suresh Shetty said, adding the government was consulting foreign experts on how best to contain the spill.
The ship was still listing deeply Monday. The MV-Khalijia-II had less damage and posed less risk; its cargo wasn't disclosed.The Jawahar Lal Nehru port was closed at least until Wednesday because of the collision and spill.

Government officials in coastal areas near Mumbai have been asked to test sea water in their area to check how far the oil may have spread, Chhagan Bhujbal, another senior minister told reporters.The captains of both vessels have been asked to appear before local officials to explain how the collision happened, police said.At least 250 containers from the damaged vessel fell off and port officials were trying to salvage them to avoid navigational hazards to other ships, officials said.Crews from both vessels were rescued without any serious injuries, Nambiar said.
Source; MUMBAI, India (AP) —