Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, February 17, 2012

Posted by BM. on Thursday, February 16, 2012

Posted by BM. on Monday, February 13, 2012

Ndivyo ilivyotokea, ameshakufa na hawezi kurudi tena. Tumebaki na sauti na picha zake nyingi. Whitney Houston amefariki mjini Los Angeles nchini Marekani akiwa na umri wa miaka 48.
Kifo kilimkuta akiwa katika hoteli ya Berverly Hilton mjini Los Angeles saa tisa na dakika 55 za mchana akiwa anajitayrasha kwa tamasha ya mkesha wa sherhe za kutolewa tunzo za Grammy. Sababu za kifo hazijajulikana mara moja lakini polisi wanasema uchunguzi unafanyika ingawa suala la madawa ya kulevya linatajwa tajwa.
Kufuatana na ukurasa wake rasmi wa tovuti inaelezwa kwamba Whitney amekua akipambana na tatizola madawa ya kulevya kwa miaka kadhaa, na alifanikiwa kuuza album, video na rikodi milioni 170 za nyimbo zake. Habari za kifo chake kimezusha wimbi mkubwa wa risala za rambi rambi katika kurasa za kijamii, kutoka mashabiki, marafiki na jamaa zake.
Whitney alisjinda tunzo mbili za Emmy na sita za Grammy pamoja na mamia ya tunzo za heshima. Anabaki kua mwanamuziki pekee kuweza kshikilia nafasi ya kwanza mara saba mfululizo katika orodha ya muziki bora 100. Alicheza katika filamu kwa mara ya kwanza katika mchezo wa Bodyguard mwaka 1992 na kufanya vizuri. Kuanzia sasa tutanza kufuatilia wengine wanaomuiga Whitney kama huyu Leona lewis, msikilize...

Kwaheri W.H.

Posted by BM. on Friday, February 10, 2012

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 70 ametapeliwa fedha zinazokaribia Yeni Millioni 4.5 wakati wa kuhamisha fedha kwenye benki. Polisi walisema jana Alhamisi kuwa utapeli huo ulifanywa mtu mmoja au timu ya matapeli iliyojifanya kumjumuisha mjukuu wa bibi huyo na mwakilishi wa kampuni ya kadi ya mkopo .
Mwanaume mmoja anadaiwa kumpigia simu bibi huyo mkazi wa jiji la Nagoya siku ya jumatatu saa mbili usiku akijifanya kuwa ni mjukuu wake akimwambia kuwa amebadili namba yake ya simu.
Polisi wamesema kuwa simu ya pili kwenda kwa bibi huyo ilipigwa siku ya jumanne saa 3 na nusu asubuhi ikipigwa na mtu aliyejitaja kuwa ni mwakilishi wa kampuni inayohusika na kadi za mikopo’credit Card ‘ na mtu huyo alimwambia huyo bibi kuwa mjukuu wake alikopa yeni million mbili na deni hilo linatakiwa lilipwe hadi kufikia jioni ya siku hiyo na kumtaka bibi huyo kuzungumza na mjukuu wake kupata udhibitisho juu ya suala hilo.
Polisi wanasema kuwa mwanamke huyo aliingia mtego kwa kupiga namba ya bandia aliyopewa na matapeli siku iliyopita na mtu aliyejifanya kuwa mjukuu wake alithibitisha deni hilo na kumuomba amsaidia kwa kuhamisha kiasi hicho cha fedha kupitia kwenye eneo la maduka ya karibu kipitia mashine za fedha za ATM.
Bibi huyo alikwenda hapo na kuhamisha fedha hizo zilizofikia yeni million 4.499. Ambazo kwa fedha za kwetu ni sawa na Shillingi za kitanzania takriban Millioni 89.
Kulingana na msemaji wa Kikosi cha Polisi baada ya hatua ya mwisho ya uhamishaji fedha kukamilika , aliwasiliana na mtoto wake na ndipo alipogundua kuwa alikuwa ameingizwa mkenge kwa kuhamisha fedha kwenda kwa matapeli.
Source: http://www.japantoday.com

Posted by BM. on Friday, February 10, 2012

Eneo la kaskazini mwa Japani limeshuhudia kudondoka kwa theluji nzito hususan mwishoni mwa juma lililopita na wakati huu pia na kuleta hali ya taharuki miongoni mwa wakazi wa huko.
Vifo vilivyotokea vilivyo na uhusiano na hali hiyo ya baridi kali na theluji imefikia watu 83 hadi kufikia jana jioni siku ya alhamisi nah ii ni kwa mujibu wa Shirika linalohusika na menejimenti ya majanga ya asili na moto ya hapa Japani. Shirika hilo limesema kuwa jumla ya watu 1,184,wamepata majeraha.
Kati ya watu 83 waliofariki, 60 kati yao walifariki wakati wakiondoa theluji katika mapaa ya nyumba zao au barabarani. Theluji nzito iliyoanguka kwenye majengo na maeneo mengine yamewaua watu 15 na watu wengine wanne walikufa kwenye maporomoko ya theluji ikiwa ni pamoja na eneo maarufu la kitalii lenye chemchemi ya maji moto .
Shirika hilo la maafa limesema kuwa ajali za barabarani pia zimetokea kutokana na kuanguka kwa theluji kiasi cha kuwafanya madereva wasionane vyema wakiwa barabarani.
Hata uwanja wa ndege wa Hokkaido inabidi usafishwe ili ndege iweze kutua na kuruka(Angalia picha)
Mashirika ya Utabiri wa hali ya hewa yanatabiri kuwa theruji yenye kimo cha sentimeta 60 centimeters huenda ikaanguka katika baadhi ya maeneo ya Hokkaido katika kipindi cha saa 24 kuanzia usiku huu , siku ya Ijumaa.
Katika eneo la Sukavu , mkoani Aoomori ambako hali ya hewa imezidi kuwa baridi na kufikia hasi 12.8 leo Ijumaa zaidi ya kimo cha mita 4 za theluji zimetanda ardhini.

Posted by BM. on Friday, February 10, 2012

Kwa miaka mingi nimekuwa nikiusikia wimbo huu lakini nilikuwa sijui maana yake leo nimeelewa na hivyo kunifanya niupende zaidi na zaidi. JB Mpyana anazungumzia ukweli wa maisha ambao una mafunzo. Hutajuta ukiusikiliza wimbo huu kisha kufuatilia maana yake. Thanks Pius Mikongoti nchini Malaysia na Shahibu Thabit kwa tafsiri.

“Kwa wasiojua lugha iliyotumika humu JB Mpiana alikuwa akiongelea mapenzi ya sasa akiwalalamikia akinadada akisema kuwa yapo wapi mapenzi ya ukweli ya enzi za mababu zetu ambapo watu walikuwa wakipendana kiukweli tofauti na siku hizi ambapo akinadada wamekuwa wakichagua wanaume kila mtu anataka mwanaume aliyesoma, mwanaume alina kazi nzuri, mwenye pesa, inakuwaje kwa wale ambao hawajasoma? Inakuwaje kwa wale ambao hawana kazi nzuri na hawana pesa?
kiujumla ameongelea mtaguso wa mapenzi wa sasa ambapo nadharia nzima ya mapenzi ni unanini? wewe ni nani? na dhana hii ndio inayojenga mapenzi kwenye ulimwengu wa sasa. Hii si tafsiri ya neno kwa neo ni majumuisho:-

L’amour est-ce aimer ou etre aimer? Bien que L’amour soit Le symbole d’un sentiment partage, etre aimer n’est jamais le signe d’un bonheur parfait = Je mapenzi ni kupenda au kupendwa? ingawa mapenzi ni ishara ya kubadilishana hisia, kupendwa kamwe si maana ya faraja iliyokamilika.
Bolingo eza maladie mabe dokotolo nango motema symptoma nango souci, kasi kisi nayango se presence ya motooyo ozali kolula, Lokola nalula masiya ye nde kisi nangai= Mapenzi ni ugonjwa mbaya, Dalili yake ni mawazo lakini dawa yake ni kuwepo kwa umpendaye,kama navyompenda Masiya(Yesu) ndio dawa yangu.

Bolingo lokola maladie contagieux tuna na bamoureux decus tuna na B’aveugles d’amour surtout na badivorces, Bakopesa yo temoignage na bango okoyoka mawa, okoyoka ngolo, okotikala stupefart, se kokamwa kamwa mama, se koimbaimba mama, se kotuna tina nzambe akela L’amour = Mapenzi kama ugonjwa wa kuambukiza lazima uwaulize waliokosa kupendwa, waulize vipofu wa mapenzi, waulize walioachika watakupa ushuhuda wao, utawaonea huruma,utakarahishwa, utastaajabika, Utakuwa unashangaashangaa mama, na kuimbaimba na kujiuliza kwa nini Mungu aliumba mapenzi.

Yango na po na nga Amida, hata na pasi tokovanda, hata bikebi tokoliya hata thomson tokotonda. Yesu kutu mwana ya nzambe babota ye na nandako ya mpata, Kasi mokili oyo ya tata naye, Likolo nase ya bango, kamweve o makamwisi mama = Kwa hiyo nimemchagua Amida katika mashaka tutaishi, hata samaki(thomson) tutakula tutashiba, Yesu ambaye ni mwana wa Mungu alizaliwa katika zizi la wanyama. Lakini dunia hii ni ya Babaye, mbingu na ardhi ni vya kwao Usishangae maajabu.

Na Kin Liboso ya kolinga moto bakoma kotuna ofandaka wapi, A biso tovandina mwalekwa nani akolinga biso mingi baboya bango na bango, Mosika eleki, bangungi baleki Taxi kutu eboya bango = Kinshasa kabla ya kumpenda mtu wamekuwa akiuliza unakoishi, Ah sisi tunaoshi Malekwa (Manzese,Uswahilini) nani atakaetupenda. Wengi wamekataliwa eti ni mbali mno mbu wamezidi huko hata Taxi haziendi huko.
Basusu liboso ya koloba Oui” bakoma kotuna otangaka wapi, Ah biso tubuka Bic mwa kala nani akolinga biso, Tika tokosa hata kokosa, Nga nazali graduet, Nga nazali licencie, Nga nazali enginieur, mpo balinga nga mama = Wengine kabla ya kusema ndio” huuliza ulikosoma wapi Ha sisi tuliovunja kalamu (Bic)yaani (kuacha shule) toka siku nyingi nani atatupenda, Wacha tudanganye mimi nina degree, mimi nina shahada ya juu, mimi mkandarasi ili tupendwe.

Basusu liboso ya kolinga moto bakoma kotuna de quele famille es-tu? Ah biso famille ezanga riche nani akolinga biso nzambe ya mpungu bandela mokili oyo otunaka mokomoko soki nani akolinga kobotama lisusu na famille ya pauvre. = Wengine kabla ya kumpenda mtu huuliza umetokea katika familia ya namna gani? Ha sisi familia fukara nani atakayetupenda,Baba Mungu rdia maumbile halafu muulize kila mtu kama yupo atayekubali kuzaliwa tena katika familia ya kimaskini.

Passe na nga eleki mabe yango naeffacer basouvernir nyoso ya mabe na bango nanga, memoir nanga eyebi kaka kombo ya Amida Chaty naye nde pelerinage edainayo petola nga mama sukolangamama, salisa nga nabika. = Maisha yangu yaliyopita ni mabaya ndio maana napenda kufufa zote mbaya kwenye ubongo wangu. Kumbukumbu yangu yajua tu jina la Amida Chaty Nimekuja kwako kama mpitaji,nitakase,nisugue nisaidie nipone.

Nalinga mindele,Bayindo,mikuse, milayi nalinga mike mpe minene, kasi chancelier wapi alatisanga palata ata bronzo hatanatolo, soit disant nga se amoureux,ancien de saio asala kala, roi de guere O mosala mpunda mama = nimependa weupe na weusi warefu na wafupi wembamba na wanene yupo wapi afisa zawadi hata medali ya chuma kifuani ieleweke kuwa mimi ni mpenzi mkongwe wa Saio( aliyepigana vita vya Saio mfalme wa vita Kazi isiyo na Mshahara……”

Posted by BM. on Tuesday, February 07, 2012

Posted by BM. on Monday, February 06, 2012

Posted by BM. on Sunday, February 05, 2012

Heri ya Maulid Nabiy S.A.W.
Wapenzi wa Mirindimo hususan waislamu wenzangu, nawatakia maadhimisho mema ya siku hii ya kuzaliwa Mtume wetu mtukufu Muhamad SAW..Mungu awajaze Kheri

Posted by BM. on Sunday, February 05, 2012

Bibi wa miaka 84 amenusurika kifo baada ya kufunikwa na theluji nzito kwa zaidi ya saa nne mfululizo. Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi , tukio hilo limetokea hatua chache kutoka makazi yake , eneo la Mogami , mkoa wa Yamagata hapa Japani.
Bibi huyo anayefahamika kwa jina la Kikuto Saito, aliwaambia Polisi kuwa aliondoka nyumbani kwake majira ya saa tano asubuhi siku ya Alhamisi iliyopita kukagua bustani ya nyumba yake na ndipo mapande ya barafu yaliyokuwa juu ya paa la nyumba yake ya ghorofa mbili yalipomuangukia na kumfumika na kutokana na uzito wa theluji hiyo alishindwa kujikwamua.

Polisi wamesema kuwa Sato anaishi na watoto wake wa kiume watatu ambao wakati wa tukio hilo walikuwa wametoka.
Mfanyabiashara mmoja anayefanya kazi zake kwa kuzunguka zunguka alisema kuwa jioni ya saa 10 kasoro dakika 10, anaaminika kuelezwa na jirani ya Saito kuwa bibi huyo haonekani na kulingana na habari za kipolisi jirani huyo aliingiwa na wasiwasi na ndipo walipomuona akiwa amefunikwa na mabonge ya barafu. Polisi wamesema kuwa ni uso tu ulikuwa ukionekana , jambo ambalo lilimfanya aendelee kuishi hadi alipookolewa.
Bibi huyo Bi. Saito alipelekwa hospitalini eneo la Shinsho ambapo madaktari walisema kuwa alikuwa akipewa matibabu ya kushindwa kupumua vyema lakini afya yake inaelezwa kuwa ni njema na kwamba anatarajiwa kutolewa hospitalini mwisho wa wiki hii.

Posted by BM. on Sunday, February 05, 2012

Kijana mmoja wa Kijapani anayeshikilia taji la kula kwa kasi Takeru Kobayashi anaelezwa kuwa amevunja rekodi ya kula vipapatio vya kuku vipatavyo 337 katika kipindi cha nusu saa katika shindano lililofanyika huko Philadelphia nchini Marekani katika ukumbi wa Wing Bowl XX, shindano lililohudhuriwa na watu takriban elfu 20.
Kobayashi amevunja rekodi iliyowekwa mwaka uliopita na Jonathan “Super” Squibb aliyekula vipapatio 255.

Mpambano huo uliofanyika juzi ijumaa uliwashirikisha waelfu ya watu waliokuwa wakifuatilia kupitia runinga zao , ambapo hatimaye Mjep akaibuka kidedea.
Na amejinyakula takriban Dola za kimarekani Elfu 20 , kitita cha haja…

AP

Posted by BM. on Sunday, February 05, 2012

Measuring blood pressure on both arms rather than only one can reveal an elevated risk of heart disease or even death, according to a study.In a review of medical literature, researchers at the University of Exeter in France found that a difference in the so-called systolic blood pressure between arms can be a useful indicator of the likelihood of heart trouble.People with high blood pressure—also called hypertension—have an increased risk of developing heart disease, stroke, kidney disease and dementia, previous research has shown.
High blood pressure is defined by the World Health Organization (WHO) as 140 over 90 millimeters of mercury or more. Mercury is used in blood-pressure gauges.
The first number measures maximum heart pressure (systolic), while the second measures pressure when the heart is in a resting phase (diastolic).
Published in the British medical journal The Lancet, the findings suggest that both-arm blood pressure checks should become standard practise, the researchers said.
The probe reviewed 28 studies with data on the difference in systolic blood pressure between arms.They concluded that a gap of 15mm of mercury or more was linked with an increased risk of the narrowing and hardening of the arteries that supply blood to the legs and feet.
It was also associated with pre-existing cerebrovascular disease, which affects blood supply to the brain and can contribute to dementia.Above this threshold, death rates due to cardiovascular problems likewise went up.
Most such cases are “clinically silent” and double-arm checks would better identify those at risk, the study said.
© 2012 AFP

Posted by BM. on Sunday, February 05, 2012

Mashabiki wa mwanamuziki wa kizazi kipya wa Bongo Fleva nchini Tanzania Abasi Kisinza maarufu kjnl 20% ambaye wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miaka saba au kulipa faini ya sh 200,000 baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi mwaka jana bado wanaendelea kuumizwa na tukio hilo.
Mashabi hao wamesema kuwa mwanamuziki huyo amekuwa kama darasa la kimaisha kwao na hivyo kitendo cha kukutwa na hatia kimewasononesha. Wakiongea na Mirindimo kwa njia ya simu kutoka Dar kuhusu sakata hilo , mashabiki hao wamesema kuwa hilo liwe fundisho pia kwa wengine wenye tabia kama zao huku wakijua kuwa wana majukumu ya kijamii.
Kwa mujibu wa habari iliyoandikwa gazeti la Habari Leo, Hakimu wa mahakama ya wilaya Kilwa mheshimiwa Arcado Chuwa alitoa hukumu hiyo baada ya kukamilisha kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili, za utetezi na mashataka. Alisema ili kuwa fundisho kwa wengine baada ya mahakama kumtia hatiani anamhukumu kifungo cha miaka saba au faini ya sh 200,000.
Awali mwendesha mashitaka, wilayani Kilwa, Thomas alisema mtuhumiwa alikutwa na madawa ya kulevya aina ya bangi gramu 20 mwaka jana mwezi wa Desemba wakati akiwa safarini kwenye kijiji cha Nangurukuru wilayani Kilwa akiwa katika gari lake.Hata hivyo 20 per cent alinusurika kutumikia kifungo kwa kulipa faini.