Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, January 19, 2009

Jamaa mmoja mkazi wa Gombolamboto Dar es salaam, amekutwa amekufa chumbani kwake baada ya kujinyonga kwa kutumia shuka aliloninginiza katika dari la chumbani kwake baada ya kuambiwa na mchumba wake kuwa anatarajia kuolewa na mwanaume mwingine. Binti huyo anayemlalamikia anasemekana ni mzuri kupita kiasi . Aliyejinyonga alitambuliwa kwa jina la Joel Joel alikutwa akiwa amekufa baada ya kujinyonga kwa kutumia shuka aliloninginiza katika dali la chumbani kwake.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa marehemu alikutwa kweli akiwa amefariki kwa kujinyonga kwa kutumia shuka aliloning’iniza kwenye dali chumbani kwake.Alisema chanzo cha kifo kilijulikana baada ya marehemu kuacha ujumbe kuwa amejiua kutokana na kusalitiwa na mpenzi wake wa siku nyingi aliyekuwa anampenda na alikuwa anatarajia kufunga nae ndoa mwaka huu.Ujumbe ulisema kuwa “Nimejinyonga kutokana na mchumba wangu ambaye nilitarajia kufunga nae ndoa kuniambia kuwa anatarajia kuolewa na mwanaume mwingine”“Tulishaahidiana kuoana mwaka huu na wazazi wa pande zote mbili walishabariki kwa matarajio yetu, najinyonga kutokana na aibu kubwa niliyoipata kwa ndugu na jamaa zanguNitaiweka wapi sura yangu tulipendana nae sana lakini ameamua kunisaliti, najinyonga kwa kuwa awali nilichaguliwa mchumba na wazazi niliwaambia nina mchumba wangu ninayempenda ambaye leo hii amenidhalilisha hivi” ByeBye ulimalizia ujumbe huo. Kifo cha mapenzi..

0 comments: