Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, January 25, 2009

Waziri mmoja mwanaume nchini Ufaransa amejitangaza kuwa yeye ni shoga na amemtaka Rais Sarkozy wa nchi hiyo amkubalie akitoa mualiko katika sherehe za serikali amualike yeye na mumewe, kwani yeye ni mchumba wa mtu.
Waziri wa Ufaransa anayehusika na ushirikianon wa bunge na serikali Roger Karoutchiunayeiona picha yake amejitokeza hadharani na kudai kwamba yeye ni shoga na ana mchumba wake wa kiume.Akizungumza na shirika la habari la Ufaransa Karoutchi alisema “Ni kweli nina mchumba wangu ambaye ni mwanaume na nina furaha sana kuwa naye. Mimi ni shoga Naongea hivi kuweka wazi kwakuwa hamna haja ya kuficha " alisema waziri huyo.
Waziri huyo anayetegemea kutoa kitabu chake mwezi januari kitakachotoa siri zake nne amesema kuwa suala hili la kuwa shoga ameliezea vizuri katika kitabu chake hicho.Waziri huyo pia aliweka bayana kuwa ameishamjulisha rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy kuwa yeye ni shoga na amemwomba akimwalika katika shughuli za kiserikali au binafsi amwalike aende na mwanaume wake kama mume wake.Shirika la habari la Ufaransa limesema kuwa katika siasa za Ufaransa waziri huyo amekuwa waziri wa kwanza kujitangaza kuwa ni shoga.Miaka 10 iliyopita Meya wa Paris Bertrand Delanoe wakati wa kampeni za uchaguzi alijulikana sana wakati huo alipojitangaza kuwa ni shoga.

0 comments: