Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, June 20, 2009

Kitendo cha kulia na kutoa machozi ni kitu kinachokubalika na tamaduni zote duniani.Unapocheka au kulia mwili huweza kupitia mabadiliko ya kikemia na kifizikia pia kutoa machozi au kucheka vyote vina faida kihisia, kimwili na ki-emotions. Watu wote tunafahamu kwamba kulia (kutoa machozi) huweza kutufanya kujisikia ahueni. Na ndio maana katika misiba inashauriwa kuwa usimkataze mtu kulia kabisa kwani hali hiyo itampa madhara ya kimwili. Wataalamu wanatuambia juu ya aina ya machozi , kwanza kuna Basal Tears:Hii ni aina ya machozi ambayo huwezesha macho yetu kuwa na majimaji kila wakati (lubiricating tears) na kufanya macho yaone vizuri. 2. Reflex Tears:Haya ni machozi ambayo huweza kutoka pale kitu kinachowasha macho kama vile kitunguu, mabomu ya machozi huingia machoni. 3. Emotional Tears; Hii ni aina ya machozi ambayo hutoka kutokana na kuguswa hisia, au tukuto moyoni. Sasa ni machozi yapi huondoa stress? Wanasayansi wamegundua kwamba Emotional tears (aina ya tatu) huwa na kiwango kikubwa cha madini ya manganese na homoni za prolactin ambazo husaidia mliaji kujisikia ahueni baada ya kilio.Ukweli asilimia 85 ya wanawake wanakiri kwamba baada ya kutoa machozi au kulia kujisikia relief na wapo relaxed.Kulia (KUTOA MACHOZI) ni moja ya njia ya asili ya kuondoa stress ikiwa ni pamoja na kucheka, kutembea, kukimbia, kupiga kelele na pamoja na kufanya ishara mbalimbali.
Sasa niliaje?JINSI YA KULIA AU KUTOA MACHOZI; Ukishaona una stress, au umekarisika au umeumizwa au una mawazo na unajisikia kutoa machozi au kulia, tafuta sehemu ambayo ni ya siri na peke yako, sehemu yenye utulivu halafu ruhusu kilio chenye machozi yanayotiririka yenyewe hadi chini kwenye cheeks (mashavu), hakikisha unaruhusu emotions zako za ndani kuhusika katika kulia kwako ili utoe machozi mengi na ya maana (content) kwani ni tiba bora zaidi na utajisikia bora zaidi na pia kujisikia kama umetua mzigo mzito ndani ya mwili wako. Na akinamama hasa tiba hii inawafaa zaidi. Tafiti za kisayansi zinaonyesha kuwa Wavulana na wasichana wote hutoa machozi kiwango sawa (au kulia lia) hadi wakifikia miaka 12. Wasichana wakifikisha miaka 18 hulia mara 4 zaidi ya wavulana. Homoni ya prolactin ambayo imo kwenye mammary glands kwa ajili ya kuzalisha maziwa hupatikana pia kwenye damu na glands za machozi. Pia kuna tofauti ya anatomy kwenye glands za machozi kwani mara nyingi mwanamke akitoa machozi huweza kutiririka hadi kwenye cheeks wakati wanaume hata machozi yakitoka bado huishia kwa wao kujifuta bila kutiririka kama wenzao wanawake. Pia wanawake wanapokabiliana na frustration, stress, matatizo binafsi na mabadiliko ya homoni hasa yanayosababishwa na ujauzito, kuwa katika siku zake, menopause hivi vyote huweza kusababisha machozi kutiririka. Na hata kutofikia malengo ambayo kwao wanayaona ni “lazima kuyafikia”. Hebu muelezee mwenza wako linalokusumbua pengine hutalia ama ukilia kidogo tu …sawa. Na kama hulii kabisa hapo sasa unaweza kuushia kujiua kwa jambo dooogo! ...Haya nawe anza basi....!take 5 mdau , Lazaraus M.

0 comments: