Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, June 19, 2009

Watu zaidi ya 20 wameuwawa kwenye mlipuko huo katika Hoteli ya Beledweyne, kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.akiwemo Waziri wa Usalama wa ndani wa nchi hiyo Omari Hashi Aden *Pichani mwnye ndevu nyeupe”.Miongoni mwa waliouwawa ni maafisa kadhaa wa Kidiplomasia wa Somalia. Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed amelaumu kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabaab , ambalo pia baadaye lilikiri kufanya shambulio hilo. Kundi hilo linaaminika kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al -Qaeda. Siku ya jumaatano watu 10 walikufa wakati kombora liliporushwa kwenye msikiti mjini Mogadishu. Katika shambulizi la jana Alhamisi , walioshuhudia walisema mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua gari lililojaa mabomu kwenye hoteli ya Medina , mjini Beledweyne, yapata Kilomita 400 kaskazini mwa Mogadishu. Abdulkarim Ibrahim Lakanyo, balozi wa zamani wa Somalia nchini Ethiopia pia ameripotiwa kuwa miongoni mwa waliouwawa. Bw. Aden alihamia mjini Beledweyne hivi majuzi, mji ulioko karibu na mpaka wa Ethiopia, katika jitihada za kukomesha wanamgambo wa Kiislamu wasiendelee kuthibiti maeneo mengi zaidi.
Raisi wa Somalia akiongea na waandishi wa habari mjini Mogadishu juu ya tukio hilo.Picha ya chini hapo ni Mmoja wa wanamgambo wanaoipinga wanaoipinga serikali ya Somalia..

0 comments: