Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Wednesday, September 30, 2009


Vuta tafakari kwa kibao hiki cha Tabu ley kiitwacho Bebe!

Posted by BM. on Wednesday, September 30, 2009


Nimepokea e-mail na nimeona nikuonyeshe huenda itakufaa;
HUGE VIRUS COMING!!! PLEASE READ & FORWARD
Hi All, Get this E-mail message sent around to your contacts ASAP.
PLEASE FORWARD THIS WARNING AMONG FRIENDS, FAMILY AND CONTACTS! You should be alert during the next few days.. Do not open any message with an attachment entitled 'POSTCARD FROM HALLMARK,' regardless of who sent it to you. It is a virus which opens A POSTCARD IMAGE, which 'burns' the
whole hard disc C of your computer.

This virus will be received from someone who has your e-mail address in
his/her contact list. This is the reason why you need to send this e-mail
to all your contacts It is better to receive this message 25 times than to
receive the virus and open it. If you receive a mail called' POSTCARD,' even though sent to you by a friend, do not open it! Shut down your computer immediately.
This is the worst virus announced by CNN. It has been classified by
Microsoft as the most destructive virus ever. This virus was discovered
recently by McAfee, and there is no repair yet for this kind of virus.
This virus simply destroys the Zero Sector of the Hard Disc, where the
vital information is kept. COPY THIS E-MAIL, AND SEND IT TO YOUR FRIENDS. REMEMBER: IF YOU SEND IT TO THEM, YOU WILL BENEFIT ALL OF US

Regards Godliving Alfred Nnyari ,IT Officer ,Catholic Relief Services Daresalaam/Tanzania Cell: +255 754 953 530 Email: galfred@tz.earo.crs.org Web: www.crs.org ; Kama una la ziada tuwasiliane ili tuwajulishe wana-wa-nchi.

Posted by BM. on Wednesday, September 30, 2009


Utaalamu wa kupanga chakula kunako sahani ...hii inapendeza au!

Posted by BM. on Tuesday, September 29, 2009


swali kwa wajuzi; Ukitaka kubadili maneno hayo ya Tatoos unafanyaje?.

Posted by BM. on Tuesday, September 29, 2009

Kilaji kwa watumiao. Nimetembelewa na Mjapani mmoja Hiroshi Ikeuchi ambaye kwa mujibu wa maelezo yake anaipenda Tanzania kuliko mfano. Amefanikiwa kutembeleaa nusu ya mikoa ya Tanzania na anaongea Kiswahili vizuri. Alipofika nilimpa zawadi baada ya kuitaja kuwa ni kifaa anachokipenda sana. Konyagi.
Zawadi kwa mgeni...du ashushe mikono ndio itakuwa ..imijibu.

Posted by BM. on Saturday, September 26, 2009


Ana nini huyu... anabip!

Posted by BM. on Saturday, September 26, 2009

kuna Vijiji maalum vya wamasai mkoani morogoro katika wilaya ya Mvomero ambako kila mnada wa Ngombe ukifanyika ...lazima Nyama nyingiene ichomwe na kuliwa na wadau..fuatilia raha ya minada hii hasa kwa wapenda nyama! chagua mofu hapo!
Utaalamu wa kuoka nyama!

Posted by BM. on Friday, September 25, 2009


Watafiti wanasema kwa mara ya kwanza chanjo ya UKIMWI iliyofanyiwa majaribio imeweza kupunguza uwezekano wa kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo.Chanjo hiyo ambayo ni mchanganyiko wa chanjo mbili zilizofanyiwa majaribio hapo awali, iligaiwa kwa watu 16,000 nchini Thailand.Watafiti hao wamesema imepunguza kwa takriban theluthi ya hatari ya kuambukiza ukimwi, virusi vinavyosababisha ukimwi.Imesifiwa kuwa ni hatua muhimu hasa katika nyanja ya kisayansi, licha ya kuwa chanjo hiyo bado ina safari ndefu ya kutumika duniani kote. Utafiti huu ulifanywa na jeshi la Marekani na serikali ya Thailand kwa zaidi ya miaka saba kwa watu waliojitolea.Watu hao waliojitolea walikuwa wanawake na wanaume wa kati ya umri wa miaka 18 hadi 30 katika maeneo yaliyoathirika sana na ugonjwa huo huko Thailand. Hata hivyo utafiti unaendelea kuona kama inaweza kutumika katika mazingira ya Afrika. Hii inatajwa kuwa ni hatua kubwa ya kisayansi.

Posted by BM. on Friday, September 25, 2009

Komredi Reginald Ndesika akifuatilia burudani ya Muziki kutoka kwenye mkanda wa wana msondo Ngoma OTTU. Jana Alhamisi, Hapa Tokyo Japani.
Hapo!
Haya fyotoa!

Posted by BM. on Tuesday, September 22, 2009


Angaria tarenti za hawa jamaa...ze Comedy picha hizi ni wakati wakiwa EATV.. .ukimaliza moja unaweza kubonyeza nyingine ukaendelea kujisevu taratibu .haya bonyeza hapo juu.!.

Posted by BM. on Tuesday, September 22, 2009


Safari hiyo lakini hatari!

Posted by BM. on Tuesday, September 22, 2009


Au..

Posted by BM. on Tuesday, September 22, 2009


Kila mahali kuna viwango vyake...hiki ndicho kiwango cha hapa kwetu ...ulipita hapo au uliruka!

Posted by BM. on Sunday, September 20, 2009


Kwa furaha na unyenyekevu mkubwa nakutakia mtazamaji wa blog hii kila la kheri katika sheehe hizi za kukamilisha mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Katika Kipindi cha Mfungo tumejifunza Kujua nafasi ya binaadamu katika dunia hii, tumejifunza kuvumilia, kusamehe, kujali na kujumuika. Na tuanze upya basi. Pokea mkono wa Eid el fitri nikijua unajali na unaelewa. Eid Mubarak!

Posted by BM. on Thursday, September 17, 2009


Hapa vijana hawa wanaonekana wakifanya kazi katika mradi wao wa kukuza mikoko katika kijiji cha Utange-Majaoni huko Mombasa, Kenya , bila shaka Tanzania tunaweza kujifunza kutoka kwao.Mwewe take 5.

Posted by BM. on Thursday, September 17, 2009


Du!... nimesikia wimbo kupitia redio moja ya Bongo ... online wimbo unaitwa V.I.P uliotungwa na Hayati Jerry Nashon Dudumizi -Pichani,akiwa na vijana Ochestra wakati huo. Kama wewe ni kijana wa zamani na unafuatilia nyimbo za kipindi hicho utamkumbuka bila shaka . Mungu ailaze roho ya marehemu peponi amin.

Posted by BM. on Thursday, September 17, 2009


Mwakilishi wa Tanzania katika Big brother Africa –BBA kule Afrika Kusini Elizabeth Gupta ameitumia siku yake ya nne Alhamisi leo ndani ya jumba La BBA katika kinyanganyiro cha siku 91. Binti huyo mwenye miaka 21 , mtangazaji wa TV aliwahi kushiriki katika mashindano ya Miss Tanzania na akawepo kwenye zile nafasi 10 za Mwanzo. Historia yake inaoonekana kuwa aliwahi kuishi Hungary. Unaweza kuangalia jinsi alivyoingia katika Jumba la BBA siku ya kwanza kupitia mtandao huu hapa; http://www.mnetafrica.com/bigbrother/video/browsevideo.aspx?Vid=17784
Na bila shaka kuanzia hapo unaweza kufuatilia matukio mbalimbali ndani ya mjengo huo na hatimaye ukampigia kura yako

Posted by BM. on Wednesday, September 16, 2009


Mdada mjasiriamali. Anayeishi hapa Japan akiwa safarini kwenda mlima Fuji! Mrefu kuliko yote nchini Japani. Take 5. Hebu fuatilia habari zake kupitia: http://mumyhery-jp.blogspot.com , uweze kuchati naye katika masuala ya fashion & design na biashara kwa ujumla, na kuziona bidhaa mbali mbali zinazopatikana mumyhery collection. Kuna mjasirimali pia katika fani ya Muziki.
Mwanamuziki wa kitanzania mwenye historia iliyotukuka duniani kwa kanda hii yetu Fresh Jumbe mkuu akiwa katika Picha na Mwanamuziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania Lady Jay Dee alipotembelea nchini Japani mwaka uliopita. Fresh anafanya kazi zake za muziki nchini japani. Take 5 mgosi!Ukitaka kujua ratiba za show zake na habari nyingine pita kwenye Official website yake inayojulikana kama : www.freshjumbe.com

Posted by BM. on Tuesday, September 15, 2009


Nchini Afghanistan vitendo vya kuoa watoto wadogo vimetia fora na hivyo kulalamikiwa na watu wanaokataa udhalilishaji wa watoto. Pichani mzee huyo ana miaka 81 ameoa mtoto wa miaka 13 na hiyo ni siku ya harusi amepozi kupiga picha na bi harusi...du Wazazi wa watoto wa kike inasemekana huwaozesha watoto wao hata wakiwa na miaka nane kama huyu kwa watu wazima ili wapewe fedha za kujiendeshea maisha. Pamoja na vita kila kukicha lakini pia kuna vituko visivyokwisha. Kama hayo hayatoshi huko Malaysia nako kuna vituko.

Bibi mwenye umri wa miaka 107 wa nchini Malaysia ambaye alishaolewa na kuachika mara 21 amesema yuko tayari kuolewa na mwanaume mwingine kwa mara ya 23 kwasababu anahofia kuwa mume wake wa 22 anayeishi naye hivi sasa anaweza kumkimbia na kutafuta mwanamke mwingine mwenye umri mdogo.Mume wake wa 22 anayeishi naye hivi sasa ambaye miezi miwili iliyopita alikamatwa akitumia madawa ya kulevya.Amemzidi umri mume wake takriban kwa miaka 70.

Bibi Wook alisema kuwa angependa kusherehekea sikukuu ya Eid el-Fitr wiki hii akiwa pamoja na mumewe na kama ikibidi basi aolewe na mume mwingine ili amliwaze wakati wa sikukuu.Muhhamad alifunga ndoa na bibi Wook miaka mitatu iliyopita akisema kuwa urafiki wa karibu na heshima uligeuka kuwa mapenzi ya kweli. Eeh...Afadhali!

Posted by BM. on Tuesday, September 15, 2009

Picha inayomuonyesha Marehemu Mohamed Mpakanjia na Mkewe ambaye pia ni Marehemu Amina Chifupa ,enzi ya uhai wao
MFANYABIASHARA maarufu na mtu mashuhuri katika fani ya michezo na Burudani nchini Tanzania Mohamed Mpakanjia amefariki dunia leo katika hospitali ya jeshi la Lugalo jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana katika hospitalini hiyo ambayo pia alifia aliyekuwa mkewe Amina Chifupa, Mpakanjia amefariki dunia katika hospitali hiyo majira ya saa saba mchana jana jumatatu. Taarifa zinasema kuwa Mpakanjia alifikishwa hopitalini hapo jumamosi iliyopita kutokana na kusumbuliwa na homa ya mapafu kwa jina jingine Nimonia. Chanzo hicho kutoka hospitalini kilichokaririwa na vyombo vya habari vinggi nchini Tanzania kinasema kuwa alipofika hospitalini hapo alionekana mwenye afya njema lakini hali yake ilibadilika ghafla na mauti kumfika.
Katika uhai wake Mpakanjia alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoa mchango mkubwa katika maendeleo ya michezo na burudani hasa kutokana na kusaidia wasanii, wanamuziki na bendi nyingi za muziki hapa nchini. Alikuwa mfadhili mkuu wa bendi ya DDC Mlimani Park 'Sikinde', Tanzania One Theater 'TOT Plus' na pia alidhamini albamu za pamoja za wanamuziki Ramadhani Masanja 'Banza Stone', Ally Choki na kiongozi wa Msondo iitwayo 'Sisi ndiyo Sisi' ya mwaka 2005. Kwa upande wa sanaa alitoa mchango mkubwa kwa kuwasaidia wasanii wengi wa sanaa ya filamu na maigizo kwa kuwawezesha kifedha kukamilisha kazi zao hizo. Mungu ailaze roho yake pema peponi. Amina.

Posted by BM. on Monday, September 14, 2009


Mtu mmoja ambaye alisimamisha gari lake katika eneo la kuegeshea gari kandokando ya barabara kuu moja katika jiji la Hokuto mkoa wa Yamanashi hapa nchini Japani…kwa lengo la kubadilisha tairi lake baada ya kupata pancha alikutwa na mauti baada ya gari jingine kumgonga kwa nyuma na kufariki papo hapo.Tukio hilo limetokea jana jumapili saa 10 na dakika 20. Mtu huyo ametambuliwa kwa jina la Tsutomu Yasuda na ana miaka 59 alikuwa safarini kuja hapa Tokyo. Abiria watatu na dereva wa gari iliyosababisha ajali wamejeruhiwa na Polisi wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Kwenye highways , uangalifu ni muhimu…japo ajali haina kinga

Posted by BM. on Monday, September 14, 2009

Katika Kumbukumbu za wapenda muziki wa Kiarabu hawawezi kuwasahau waimbaji utakaowaona kwenye You tube hii. Hawa wana uwezo wa kukariri kibwagizo tu cha nyimbo , lakini mashairi huyaingiza hapo hapo kadri mzuka wa muziki unavyopanda. Katika hafla hii waimaji hawa wa kiume na wakike walikuwa wakishindanisha pumzi zao.Chukua muda wako uangalie vipaji hivi kutoka dunia ya kiarabu.
Unaona nyimbo ya kiarabu zinavyochezwa ..hebu nawe jaribu taratibu...

Posted by BM. on Monday, September 14, 2009


If you want to start a relationship with a girl, the first thing to do is to check if she's really interested in you. The problem is that body language is not always a safe way to find this out. There are some girls who can imitate the body language of an interested girl, but they are not interested in you. They will only play with your heart and/or use you!!! These are some techniques to detect these types of "users" and that help to protect you from being used:

1. First check out if she will give you her phone number, and if this is her true number! If she won't give you her number or it is a false one, forget her!

2. Check out if she will go on a date with you. If she is "too busy" all the time or something like that and it is impossible to get a date with her, then she is not interested.

3. If she is asking you to buy her a drink the first time you flirt with her, then alarms should go off in you head. Don't allow her to use you this way! Amarula, Safari, Serengeti eti nina kiu kweli leo!!
4. If you are on a date with her do something where you don't need to spend too much money and don't bring her a present on the first date. You want her to love you as a person and not to love your presents or the fact that you pay for everything. Try to keep the temptation of using you as low as possible.
5. After the first (or maybe the second even the third) date tell her something like "Well, I really enjoyed...." and so on and "Maybe we can do this again next time. You can call me..." It is important to tell HER to call YOU not beeping!!!!!because she will only call you if she is interested.

6. Analyze if she only wants do things that make her happy. For example, if she is calling you only if she wants to have someone to repair her car, fixing here fence or something like that, but never calls you for a normal date, then think about it...

7. If you find out that she has a boyfriend or if she even tells you that... FORGET HER! She may pretend that she is interested in you and that she might leave her boyfriend for you, but she will NEVER DO IT!!! Au unasemaje? ......

Posted by BM. on Monday, September 14, 2009


Rafiki yangu mmoja wa Tz kanitumia hiyo picha akisifia sana hayo marembo ya "Vikuku" ambazo ama zinakuwa shanga ama mikufu. Weye unasemaje.

Posted by BM. on Saturday, September 12, 2009


Safari kuelekea nyumbani kwa Mwenyekiti wa Tanzanite , Japani lazima ufike hapa Kunitachi.Naelekea huko sasa nina mwaliko..

Lango la kusini la kituo cha treni cha Kunitachi, nimekutana na teksi zikiwa katika foleni ya kistaarabu....Inapendeza.

Mwenyekiti wa Jumuia ya watanzania wanaoishi Japani inayojulikana kama Tanzanite alipata wageni nyumbani kwake kufuatia mwaliko wake alioutoa kwa ajili ya Futari.
Kati ya waalikwa mashuhuri ni ni Mr. Tutuba na Mr. Herman Mpangile wakiwa katika vyuo vikuu hapa Japani kuongeza maarifa. nami nilialikwa . Pamoja na futari nilipata kusikiliza busara ya viongozi wetu. Ilikuwa hafla ya kufana iliyoandaliwa na Dr. Simba na Mkewe Fatma. Pitisha macho. Hapo menyu ya leo ya Futari , Nyumbani kwa Mwenyekiti.

Mama mwenye Nyumba ndiye aliyefanikisha haya yote..take 5 Mrs. F.Simba
Mwenyeji wetu Dr.Ally Simba Akiwa nasi katika risq iftar.

Wageni waalikwa:Kutoka kushoto Bm, Tutuba na Herman Mpangile . Wakubwa wananoa vichwa katika Vyuo vikuu hapa japani..lakini leo pamoja nao tulikuwa tukifutariswa kwa Mwenyekiti.

Raha ya funga ...futuru Hongereni Mr.and Mrs. Simba.

Posted by BM. on Saturday, September 12, 2009


Kijiji cha Lusanga kipo wilayani Mvomero mkoani Morogoro. Ni kijiji chenye historia ndefu na kimekuwepo hapo miaka mingi iliyopita. Moja ya sifa za kijiji hicho ni ardhi iliyo na rutuba. Mazingira asili hayajaharibiwa hata chembe . Mgosi Peter Omari alikuwa hapo na akafyotoa picha na kuzimuvuzisha kwenye Mirindimo. ...Nimewakumbuka ze Comedy!

Virgin Land; Kiswahili chake Kiguumu.Oke... Hapajalimwa hapo tangu paumbe....au!

Wazee wanatuambia minazi hiyo imekuwepo kwa miongo mitano sasa , miaka 50. Lakini hadi leo madafu, nazi na pombe ya mnazi inapatikana kwenye minazi hiyo hapo Lusanga.

Miti asili kama hii imetapakaa katika kijiji hicho na kutengeneza mandhali ya kipekee

Ubunifu wa watoto wa Lusanga.

Posted by BM. on Saturday, September 12, 2009


FUNGA: Mazoezi ya kimwili na kiimani.

Posted by BM. on Friday, September 11, 2009


Wajasiriamali wa Segera , Mkoani Tanga , Tanzania na biashara ya matunda.

Posted by BM. on Friday, September 11, 2009


Mtoto wa miaka nane anayesoma shule ya msingi Shiba-minami elementary katika jiji la Kawaguchi hapa Japani amefariki jana Alhamisi baada ya kuanguka kutoka kikorido cha ghorofa ya nne cha shule hiyo hadi chini ya jengo karibu mita 12. Baada ya tukio hilo la kusikitisha Mtoto huyo alikimbizwa hospitalini lakini saa nne baadaye alifariki dunia. Kwa mujibu wa Polisi tukio hilo limetokea saa tisa na nusu za jioni na inasemekana hakukuwa na wanafunzi wala wafanyakazi shuleni hapo alipokutwa na maafa hayo . Inasemekana wazazi wake walimfuata mtoto wao hapo shuleni na walimuona wakati anaanguka kutoka ghorofani.Picha inayowaonyesha watoto wakitoka shuleni haina uhusiano na motto aliyefariki ingawa furaha ya watoto wakimaliza siku shuleni huenda marehemu angekuwa nayo kama angekuwa hai.

Posted by BM. on Friday, September 11, 2009

Alama ya jiji...ushanfahamu! Hili ni jiji la Yamato nchini Japani liko nje kidogo ya Tokyo...Lina umaarufu wake . taarifa zaidi baadaye. Mtaa wa madukani ..Yamato ..hukosi kitu mkubwa hapo.. Parking..Ingekuwaje kila mtu angepaki anapopataka...pasingetosha. uongo?
Simama kwanza soma maelekezo...

Posted by BM. on Friday, September 11, 2009


Nilifika Yamato!...