Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, February 20, 2010

Wadau wakijimwaya katika ukumbi wa Kiluvya Pub, Kibaha siku ya wapendao Feb 12. Aina ya muziki unaochezwa hapo, saaana ni Rhumba la kizamani. Nakuweke moja ya nyimbozinazotamba hao weekend. Bahati nzuri maandishi yana tafsiri ya kiingereza wacha nami niyatafsiri kwa kisukuma ,lugha ya kwetu.Soma kwanza tafsiri ya wimbo huo kwa kifupi halafu bofya usikilize wimbo wenyewe.
"Tumezungumza sana jana jioni,
lakini baadaye usiku usingizi uliruka kabisaa,
nilikuwa nikiuliza kama hili litaweza kuwa kweli?
Jambo ulilokuwa ukilizungumzia lilinishangaza kweli!"
"...Ninashangaa kwanini unanifanyia wivu, kwani tulikwishaachana na wewe umeoa kitambo,Huwa nakupokea mara kwa mara nyumbani nikidhani unakuja kumuona mtoto lakini cha kushangaza unaniambia eti tuwe wapenzi tena..Unajua !...siko peke yangu tena siku nyingi tu niko na Pedejzheee..."

Picha za burudani hiyo ya Valentine unaweza kubofya po kwenye mitandao rafiki hapo kwenye Kiluvya pub. Haya sasa bofya hapo chini.

0 comments: