Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, February 28, 2010

Jana Jumamosi nilitembelewa na watu muhimu sana katika makazi yangu hapa Tokyo. Ilikuwa siku nzuri na nilifaidika sana na mada zilizoongelewa nyingi zikiwa za changamoto ya kimaisha. Mmoja wao alikuwa Mwenyekiti wa Jumuia ya watanzania waishio nchini Japani TANZANITE Dr. Ally Simba. Baada ya mazungumzo kilichofuata ni kupata rizki.

Komrade Amani (Kulia) na Francis Mosongo , Afisa wa Ubalozi wa Tanzania hapa Japani (Kushoto) walikuwepo katika mazungumzo haya ya kirafiki.

Nilihemewa kwa furaha kuwa na watu muhimu na kunimegea busara zao.

Mwenyekiti, Dr. Simba na mdau Reginald Ndesika , wakipata kitu kidogo huku mijadala ikiendelea.

0 comments: