Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, February 23, 2010

Hivi sasa kuna Operesheni kali huko Afghanistan kuwasaka Wa-TALIBAN, Operesheni inayofanywa na majeshi ya NATO wakiongozwa na MAREKANI. Tuiangalie kwa njia ya picha.
Mzee huyo anayeongea anaitwa Haji Abdul mlimaji wa Afyuni -Opium kilevi kinachowapatia fedha nyingi wataliban ; hapa anahojiwa shambani kwake huko Qalanderrabad . Wanajeshi wa Marekani wameahidi kumlipa fidia kwa kuharibu mazao yake walipoteremka kwa parachuti hapo lakini kwa sharti awaambie walipo wa-Taliban. Sijui walimalizana vipi...

Mji umeteketezwa kabisa , kisibaki kitu...du aliyekuwemo na asiyekuwemo .Balaa. Eneo la Gandalobog, Afghanistani panapoaminika kuwa na makao makuu ya Wataliban. Vita si mchezo unakataa! eneo ambalo Majeshi ya Marekani wanaamini kuwa maroketi ya Taliban yanatokea. Sgt Darin Hendricks amepewa jukumu la kuiiangia ndani na kuchungulia ili kujua kukoje. kazi ipo!
Mwili wa mtu anayeshukiwa kuwa ni askari wa kundi la Taliban .Picha zote kwa hisani ya mtandao wa boston.

0 comments: