Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, March 27, 2010

Waziri Mkuu wa Japani Yukio Hatoyama akimkaribisha Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda Ofisini kwake tayari kufanya mazungumzo rasmi.(Life network)
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda amemaliza ziara ya siku tatu nchini Japani ambapo Pamoja na mambo mengine alikutana na Waziri Mkuu wa JP, Yukio Hatoyama na Waziri wa mambo ya nje Katsuya Okada na kujadiliana nao masuala mbalimbali ya ushirikiano katika sekta za Miundo mbinu na Kilimo.Katika upande wa miundombinu Viongozi hao wametia saini mkataba wa mkopo ambapo Japani itaipatia Tanzania Yeni Billioni 7 kuimarisha mtandao wa miundombinu ya nyumbani, kama anavyoainisha Mh. Pinda.



Kwa hakika hapo alikuwa anamalizia kwa kuomba usaidizi wa ujenzi wa barabara kati ya Dodoma na Babati mkoani Manyara.
Baada ya hapo alijumuika na wananchi waliopo hapa katika mkutano uliofanyika kuanzia saa mbili hadi saa tano usiku. Kwa WaTz-waliopo JP walio na picha za matukio ya ziara hii wanaweza kuzituma kwa njia ya email kwa; brmsulwa@yahoo.com ili ziwekwe ili wengine wapate kuona kilichojiri...karibu.

3 comments:

Subi Nukta said...
This comment has been removed by the author.
Subi Nukta said...

video mmetupunja mwe!

Anonymous said...

Nakubali Da subi next time mambo yatakuwa mswanooo!