Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Thursday, March 18, 2010

Eneo la kihistoria la makaburi ya kifalme yameteketea kwa moto katika mji mkuu wa Uganda , Kampala. Jengo la nyasi eneo la kasubi linaloonekana katika picha limeteketea likiwa na kumbukumbu mbalimbali za kijadi pamoja na makaburi wa wafalme wa Buganda waliotawala katika himaya hiyo kwa karne kadhaa zilizopita. Hili pia ni eneo lilitumia kama nyumba ya ibada kwa wa buganda
Raisi Museveni alikwenda katika eneo hilo na akakumbana na watu waliojaribu kumzuia na ndipo Pilisi walipoanza kupambana nao kumpa njia Museveni na ndipo watu watatu walikufa hapo hapo. wanaoipinga serikali wanadai Serikali ya Museveni inahusika na kuchomwa moto kwa eneo hilo.
Polisi wa kutuliza ghasia kwa kufyatua risasi..

Historia inaonyesha kuwa Ufalme wa Buganda ulisitishwa mwaka 1963 wakati Uganda ilipopata uhuru wake lakini ulirudishwa tena mwaka 1993 ingawa sasa kwa ajili ya kumbukumbu ya kiutamaduni na wala si kisiasa.

0 comments: