Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, May 28, 2010

Ilikuwa taarifa ya kushitusha kuwa mwanamuziki Fredy Mayaula Mayoni amefariki dunia huko Ubeligiji jana Ijumaa kwa ugonjwa wa kansa ya Ubongo. Alikuwa na miaka 64 alipoacha kuvuta pumzi. Kwa kipindi kirefu kulikuwa na taarifa za kuugua kwa mwanamuziki huyo na inasemekana alipata ugonjwa wa kupooza miaka miwili iliyopita na baadaye hali ikatengemaa.


Mie binafsi taarifa hiyo iligusa kwasababu ya kumtambua kupitia nyimbo zake kama vile Mbongou yaani pesaaa pesaa ,Mwanamuziki hyu pia aliwahi kuichezea timu ya Yanga ya Tanzania mbali na kuwa mtaalamu wa kutumia komputa.Kwa wakazi wa dar hasa wanaokaa Magomeni Mikumi watamkumbuka vyema maana alikaa maeneo hayo wakati fulani wakati baba yake akiwa ubalozi wa DRC nchini Tanzania. Moja ya nyimbo ninayoipenda sana ni Othman, kwahakika sijui maana yake , lakini nahisi wimbo huu una ujumbe mzito sana. Mungu aiweke peponi roho ya mayaula Mayoni , Amen.

0 comments: