Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, September 19, 2010

Iliyokuwa REDIO TANZANIA(RTD)...



Watangazaji wa kitambo wa RTD; Kulia Ahmed Kipozi katikati Mkewe Sango Kipozi na Kushoto Betty Mkwasa ambaye sasa ni Mkuu wa wilaya ya Bahi kule Dodoma. Kipozi na Mkewe sango walikuwa watangazaji hapa NHK Japani miaka ya nyuma. Ni hazina kubwa ya taifa katika tasnia ya Utangazaji...

1 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Hii post yanikumbusha niliyowahi kuisoma kwa Dada Subi nami nikaiandika (kuiboresha) kwangu.
Kama ulivyosema ni HAZINA KUBWA lakini kwa bahati mbaya HAZINA HII HAITHAMINIKI, HAIKUMBUKWI WALA KUHESHIMIKA.
Inanisikitisha kuwa wanaoiweka nchi pabaya ndio wanaothaminika. Wanaofuja mali ndio wanaoonekana wajanja. Lakini WAELIMISHAJI kama ninyi, kama hawa, kama wanamuziki walioimba kutangaza sera za SERIKALI kama za Gezaulole na wengine walioimba yaifaayo jamii HAWATHAMINIWI bali wanapuuzwa na kufa wakiwa maskini.
Rejea post niliyoiandika (nikiboresha ya Dadangu Subi) kwa kubofya hapa http://changamotoyetu.blogspot.com/2010/04/tunawapenda-hatuwathaminikwa-kuwa.html

Baraka kwako Uncle