Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, March 21, 2011

Mwandishi wa habari Jonas Jackson Songora , majuzi alitunukiwa shahada yake ya Pili (Degree of master of Science in International Cooperation policy) katika Chuo Kikuu cha Ritsumeikan Asia Pacific-APC baada ya kutimiza vigezo vinavyohitajika. Sherehe ya kutunukiwa nondozz hizo ilifanyika Jumamosi ya tarehe 16 , March katika Chuo hicho kilichopo eneo la Kyushu Kusini mwa Japani. Kabla ya kuja hapa Japani Jonas aliwahi kufanya kazi nchini Tanzania katika vyombo mbalimbali vya habari (Redio na Magazeti) na kwasasa anawajibika katika Shirika la Utangazaji la Japani -NHK world) Idhaa ya Kiswahili, kama mtangazaji wa kutumainiwa.
Picha; ya kwanza ameshikilia cheti chake, inayofuata akiwa na wahitimu wenzake , chini yake na wanafunzi wa kiafrika wanaosoma hapo na mwisho mwanafunzi mwenzake wa kitanzania Moses Kwabhi..

Hongera sana bro!

0 comments: