Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, April 29, 2011

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Clement Senzota Mwete Mshana kuwa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Taarifa iliyotolewa Ikulu, Dar es Salaam, juzi, Jumatano, Aprili 27, 2011, na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Bwana George Yambesi inasema kuwa uteuzi huo unaanzia Alhamisi iliyopita, Aprili 21, mwaka huu, 2011.
Kabla ya uteuzi huo, Bwana Clement Senzota Mwete Mshana alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo).


Bwana Mshana anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bwana Danstun Tido Mhando ambaye amemaliza muda wake wa utumishi kwa mujibu wa mkataba wake.


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

27 Aprili, 2011

1 comments:

Anonymous said...

KWA NIABA YA WADAU WA LUGHA YA KISWAHILI NAMPONGEZA SANA NDUGU CLEMENT MSHANA.

R.Njau
TZDAR