Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, October 10, 2011

Sekunde moja iliyopita...Mechi ya Tanzania Taifa Stars imemalizika huko Rabat na Timu ya Tanzania imefungwa kwa tabu magoli 3 kwa moja . Haabari ndiyo hiyo!
Mchezo huo ulikuwa wa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani Guinea ya Equator na Gabon. Mchezo huo ulifanyika katika kwenye Uwanja wa Marraketch.

Stars ilikuwa katika nafasi ya tatu katika msimamo wa Kundi D baada ya kujikusanyia pointi tano, iko nyuma ya vinara Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati, zenye pointi nane kila moja na ziko katika nafasi ya kwanza na pili na kwa mechi hii Morroco inapanda kileleni. Stars ilihitaji ushindi wa angalau kuanzia bao 2-0 dhidi ya wenyeji wao Morocco,ndoto ambazo hazikutimia.
Tayari timu za Senegal, Ivory Coast, Botswana na Burkina Faso
zilikuwa zimejihakikishia tiketi ya kucheza fainali hizo za Mataifa ya Afrika, na kuziacha timu zingine zikigombea nafasi 10 zilizobaki.
Pambano hilo la Stars na Morocco lilichezeshwa na waamuzi kutoka Gabon, ambao ni Gassama Bakary, Jawo Dickory, Touray Sulayman na Camara Bakary, walioteuliwa na CAF wakati Kamishna wa Mchezo ni Zoumaro Gnofame kutoka Togo. Dakika ya mwisho kipa wa Taifa stars alifanya kazi ya ziada kuzuai michomo kuingia langoni vinginevyo yangelikuwa mengii tu. lakini vijana wamejaribu!

0 comments: