Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, December 13, 2011

Moja ya mabasi 20 ya kitalii yanalojulikana kama SKY DUCK la kiamfibia ambalo linaweza kusafiri majini na katika nchi kavu.Tarehe 14 mwezi Novemba lilifanya majaribio jijini Tokyo na kuvutia watu wengi sana.
Nyuma la basi hili kun propera na bila shaka itakujulisha kuwa hili si la kawaida. Likiwa majini linakwenda mwendo wa kilometa 11 kwa sasa lakini nchi kavu linaswaga mwenda kama kawaida. Watalaamu waliobuni basi hili wamekuwa na dhana na maisha ya bata anayeweza kuishi majini na nchi kavu. Basi hili limetengenezwa kwa gharama kubwa sana unaweza kupiga hesabu. Kama uko Tanzania hebu piga hesabu (Yeni Millioni 80 x20) utapata fedha za kitanzania ni kama Tsh. 1,600,000,000 . Kwa kawaida basi jipya lisilo la namna hii linagharimu Yeni Yeni million 30.Basi hilo lina magurudumu manne linayoyatumia kusafiri barabarani

1 comments:

ray njau said...

HONGERA KWA WANAZUONI MAHIRI NA MAKINI KATIKA TASNIA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA NCHINI JAPANI.