Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Wednesday, April 22, 2009

Mzee mmoja wa Kichaga ambaye alikuwa mkali sana kwa binti yake anaamka asubuhi na kutaarifiwa kwamba binti yake ana mimba!
Mzee wa Kichaga: "Aisee we Manka,nakwenda kazini,nikirudi leo ni lazima uniambie ni nanikafanya uchafu huu"Akafoka na kuondoka kuelekea ofisini.Mchana anapigiwa simu na Mama Manka nakuambiwa kwamba yule jamaa aliyempa mimba bintiye yuponyumbani anamsubiri kwa mazungumzo!Mzee anachukua panga lake na kulinoakabisaaa kwa ajili ya kwenda kumteketeza mwanaharamu huyo.Kufika nyumbani mambo yanakuwa hivi:
Kijana aliyempa mimba binti: Mmmh!!, Mzee ni kweli mi ndiye nimempa mimba binti yako, na kusema kweli sina mpango wa kumuoa.Lakini akizaa mtoto wa kiume nitakupa Millioni hamsini na nyumba ya ghorofa eneo la Kariakoo kisha nachukua mtoto.Akizaa mtoto wa kike nakupa Millioni kumi na duka Sinza! Lakini je mzee, ikitokea bahati mbaya mimba hii ikaharibika itakuwaje?
Mzee wa Kichaga akajibu : Aisee babaangu itabidi tu umpe mimba nyingine,hakuna jinsi! Duh....

0 comments: