Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Wednesday, April 22, 2009

Milima ya uluguru mkoani Morogoro imekuwa vipara siku hizi , maji yaliyokuwa yakitiririka kutoka kileleni yameacha na ubaridi katika mji wa Morogoro umeanza kupungua ...ni uharibifu wa mazingira. Wataalamu wanasema kuwa Misitu ya milima ya Uluguru imepungua kutoka hekta 30,000 mwaka 1950 hadi hekta 20,000 mwaka huu na hii imetokana na vitendo vya uchomaji moto katika milima ya Uluguru. Amesema kupungua kwa misitu katika milima hiyo kunatokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na uchomaji moto, kilimo cha migomba pamoja na bangi na kwamba katika kipindi cha Januari hadi Oktoba mwaka huu zaidi ya hekta 200 za misitu katika milima hiyo zimeteketezwa kwa moto. Milima ya Uluguru ni muhimu hasa kutokana na kuwa na makazi ya viumbe mbalimbali ambapo wengine baadhi yao hawapatikani sehemu yoyote duniani. *(Picha na Int.P. Peter Omari)

0 comments: