Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, May 17, 2009

Hawa ni watu muhimu sana katika historia ya Tanzania. Bila shaka Mwalimu J.K.Nyerere anafahamika vizuri tu. Kuliakwake ni Bibi Titi Mohammed. Huyu ni mmoja wanawake wa kwanza kushika nafasi za ubunge na uwaziri na pia ni kati ya wanawake wa kwanza kujiunga na harakati za kugombea uhuru wa Tanganyika wakati ule , akiwa na ushujaa mkubwa kuongea majukwaani , wakati huo ilikuwa kitu cha nadra sana!
Mwaka 1969 Bibi Titi Mohammed alikamatwa na mwaka uliofuata alifikishwa mahakamani kwa kosa la kula njama ya kutaka kupindua serikali. Katika kesi hiyo, Bibi Titi alikuwa ni mwanamke pekee katika washtakiwa 7. Baada ya kesi hiyo kusikilizwa alipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha. Hata hivyo, mwaka 1972 alisamehewa na Mwalimu nyerere aliyekuwa Raisi wa Tanzania. Wote sasa ni marehemu lakini historia zao bado zi hai...

0 comments: