Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, May 17, 2009

Unweza kuamini kuwa huyo alikuwa mwanaume rijali wa kupewa mke akaamua kujibadilisha na kuwa mwanamke kama unavyomuona...Hii ndiyo dunia ya leo ya sayansi na teknolojia . Hebu fuatilia mashindano ya ulimbwende ya watu waliopata kuwa wanaume katika maisha yao yaliyofanyika huko Thailand hivi karibuni...

Kama ilivyokuwa miaka mingine, mwaka huu pia mashindano ya kumtafuta mrembo wa mashoga yamefanyika nchini Thailand yakishirikisha mashoga 30, huwezi amini kama hawa zamani walikuwa wanaume rijali. Picha za mashoga hao mwisho wa habari hii.Mashindano hayo kutokana na kutotambulika katika nchi nyingi duniani, kila mwaka hufanya nchini Thailand.Mashoga wanatambulika nchini Thailand kama jinsia ya tatu na wanajulikana nchini humo kama 'Katoey.'Huu ni mwaka wa 12 kwa mashindano hayo kufanyika na mashoga 30 walishiriki kutafuta mrembo kati yao katika mji wa utalii wa Pattaya nchini humo.Mashoga hao walipita mbele ya mamia ya watu waliofurika kushuhudia tukio hilo wakiwa wamevalia mavazi mbali mbali kuanzia viguo vya kuogelea mpaka vya kulalia.Mwisho wa mashindano hayo shoga nambari 26 aliyejulikana kwa jina la Sorawee Nattee aliibuka mshindi na kuvikwa taji lake la mrembo wa mashoga au "Miss Tiffany" kama shindano hilo linalovyojulikana.

Ukishitukizwa unaweza kujua kuwa hawa ni mashoga waliofanyiwa upasuaji wakawa hivyo...Duh!


0 comments: