Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, November 28, 2010

Je huu ni Uungwanaaa?
LAHASHA huu si uungwana
.

2 comments:

Subi Nukta said...

Nilikuwa sibanduki redioni ng'o katika kipindi cha Leornard Mambo Mbotela kila Jumapili saa sita hadi saba mchana. Na Mama alishalifahamu hilo hivyo alikuwa akitaka kazi ifanyike, basi aniambia bila kuikamilisha hiyo, leo usiguse redio. Loh loh loh, nikose kusikiliza Je, Huu ni Uungwana? thubutu, nilikuwa nafanya kazi zote chap chap.

Kingine ambacho kilikuwa hakinitoi redioni ni kipindi cha maswali na majibu kikishindanisha "shule za Upili" kilichokuwa kinakuja kabla ya Je, Huu ni Uungwana na cha tatu kilikuwa cha saa tisa u nusu hadi kumi, cha "Wimbo niupendao".

Ah, sisi tuliokulia mikoa mpakani na Kenya tumefaidi sana kusikiliza "hii ni KBC Nairobi".

Waliokuwa na TV walienda hatua moja zaidi kufaidi "KBC - Vitimbi" akina Masaku, Mama Kayaii, Ojwang, Otorong'ong' (RIP) na kile cha "Vioja Mahakamani"

www.mawio-shineshine.blogspot.com said...

Da Subi una kumbukumbu nzuri sana...Mbotela ni mtangazaji mwenye kipaji sana kwanza katika kuibua story ambayo itwagusa watu na jinsi anavyosisitiza jambo kwa kiingereza na kiswahili. Yaani kama unahusika inakugusa sana tu na utaacha. Na yule mtangazaji wa zilipendwa sijui walikuwa wakiita 'tunazikumbuka' alikuwa balaa. Kwa RTD kulikuwa na kipindi cha nipe habari cha David Wakati na baadaye sana mwanzoni mwa enzi zetu ilikuwepo Jungu kubwa. we acha tu. Thanks kwa kunikumbusha.