Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, December 12, 2010

Watanzania wanaoishi nchini Japani , wakati huu ndio wanaondoka kutoka kwenye ukumbi wa PPP karibu na kituo cha treni cha Sagamino uliopo mkoa wa Kanagawa nchini Japani walipokuwa wamejumuika kusherehea miaka 49 ya uhuru wa taifa lao la Tanganyika na baadaye Tanzania ... Mgeni wa heshima alikuwa Mh. Salome Sijaona , Balozi wa Tanzania hapa Japani.



Meza Kuu; pichani katikati Mh. Salome Sijaona , Kulia kwake Mumewe Bw.Sijaona na kushoto kwake , Dr. Ally Simba mwenyekiti wa Watanzania wanaoishi Japani.Na kulia kabisa ni Katibu Mkuu Tanzanite Mwombeji jr.

Ulikuwa mchanganyiko wa Muziki wa dansi ulioporomoshwa na Fresh Jumbe Mkuu na Bendi yake ya TANZANITE na Disco chini ya DJ Pembe. Chakula , hotuba na uzinduzi wa tovuti ya Jumuia ya watanzania hapa Japani, Tanzanite society.
Balozi Salome katika hotuba yake alikumbusha kuwa watanzania walio nje wana wajibu wa kutoa mchango wao wa kulijenga taifa lao, na wasiishi kwa kujisahau, kwani maendeleo yanaletwa na watu wenyewe. Alihimiza umoja baina ya Watz waliopo Japani na kuwakumbusha wajibu wao wa kufanya kazi kwa bidii kama wanavyofanya wajapani wenywe pamoja na utajiri walio nao.

Baadaye Mwenyekiti wa Tanzanite Dr. Ally Simba aliwahimiza watanzania ambao hawajajiunga na Jumuia hiyo wafanye hivyo kwani Umoja ni nguvu , utengano ni udhaifu. Ulifuata muziki, chakula na vicheko kila upande. Fuatilia tukio hilo kwa njia ya picha.

0 comments: