Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, March 25, 2011

Maafisa wa kijeshiwa Uingereza wakisema wamefanikiwa kuuvuruga kabisa mfumo wa jeshi la anga la Libya katika mapambano yao yanayowashirikisha mataifa kadhaa ya Magharibi ikiwa ni pamoja na Ufaransa, Marekani, Uingereza na baadhi ya mataifa ya kiarabu.Mashambulizi ya hivi karibuni yaliendelea huku milio ya makombora ikifyatuliwa kwa mfululizo.

Operesheni hiyo inatekelezwa, wakati ambapo wajumbe kutoka nchi 28 za jumuiya ya Kujihami ya NATO, wakiendelea na mkutano wao nchini Ubelgiji, wenye lengo la kujadili namna jumuiya hiyo itakavyoshiriki katika operesheni hiyo. Hali bado ni tete libya. Unaweza kuona pilikapilika za waasi wa Serikali ya nchi hiyo wanaosaidiawa na Nchi za magharibi.

0 comments: