Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, August 30, 2011

Leo ni Eid el Fitri. Jana jumanne waumini wa dini ya kiislamu wa madhehebu ya Answar suna katika eneo la Afrika Mashariki na kwingineko duniani walifanya ibada hiyo ya Eid-el fitri . Na waumini wengine wanaadhimisha siku hiyo hii leo... Eid Mubarak!
Barakat el Eid ndugu, marafiki na jamaa zangu wote kwa sherehe hizi za Eid el fitri. Nakupa mkono wa Eid, tafadhali nikubalie... Hii ni ishara ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Namuomba Mwenyezi Mungu atuzidishie mimi na wewe subra, atupe afya, atupe murua, atujaalie uvumivu , ustahimilivu, hekima , busara na ubinaadamu. Tushikamane kupitia maagizo ya Mwenyezi Mungu na atuwezesha kuachana na mabaya yaliyopita ili tusogeze mbele yaliyo mema. Blogi yako hii ya MIRINDIMO iko pamoja nawe katika hatua zote hizi. Tuombeane mema ,Inshallah.BM

(Picha mbili hapo chini ) zinawaonyesha baadhi ya waumini wa madhhab ya Answar suna wakiwa katika ibada ya Eid El-fitri jana Jumanne asubuhi katika viwanja vya Jangwani Dar es salaam. Shekhe aliyeiongoza ibada hiyo, Shekhe Juma Poli Amri akitoa mawaidha. Madhehebu mengine wataswali swala ya eid Fitri leo jumatano ...Inshallah


0 comments: