Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, November 26, 2011

Leo hapa Japani katika Chuo Kikuu cha Soka, kulikuwa na mashindano ya kutoa hotuba kwa lugha ya Kiswahili kuwania kombe la mwasisi wa Chuo hicho Daisaku Ikeda. Mashindano hayo yameandaliwa na Chuo hicho kwa uratibu wa mmoja wa wahadhiri wake Bi. Midori Uno. Haya ni mashindano ya 21 na yaliwakusanya wageni mbalimbali ikiwa ni pamoja na Balozi wa Tanzania hapa Japani Bi. Salome Sijaona , na afisa wake , wawakilishi wa Balozi za Kenya na Kongo DRC pamoja na Shirika la Utangazaji la Japani-NHK WORLD. Ma-MC walikuwa mabinti wa wawili(Angalia picha hapo chini)... Jina moja limenitoka lakini wakulia ni Kiko Sawajiri..

Balozi Salome Sijaona aliongea mwanzoni mwa hafla hii (Pichani)kwa kueleza mafanikio ya kijamii, kisiasa na utamaduni yalivyofikiwa Nchini Tanzania na eneo lote la Afrika Mashariki kwa kukitumia kiswahili na kusema kuwa lugha hiyo sasa ni ya kimataifa hivyo inapaswa kuenziwa na kusambazwa kote duniani...Amewapongeza wanajumuia wa Chuo Kikuu cha Soka kwa kuendeleza mashindano hayo...
Haya fuatilia tukio hilo kwa njia ya picha...

1 comments:

ray njau said...

WEWE UKISEMA CHA NINI MWENZIO ANASEMA NITAKIPATA LINI?