Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, December 16, 2011

Makundi ya haki za binaadamu nchini Bangladesh yamekuwa yakichagiza kutolewa kwa adhabu kali kwa mume wa binti mmoja nchini humo anayedaiwa kuvikata vidole vya mkewe vya mkono wa kulia.Polisi wamesema kuwa Rafiqul Islam,(Pichani) mwenye miaka 30 alimfanyia kitendo hicho mkewe kwasababu alikuwa amejiandikisha kuendelea na masomo ya juu bila ya kupata ruhsa ya mumuwe huyo.
Wamesema kuwa Mtuhumiwa Islam (Picha ya chini) , mfanyakazi mhamiaji alikiri kufanya kitendo hicho mara tu aliporejea kutoka uarabuni.Hata hivyo hakuna ushahidi ulio wazi juu ya kuhusika kwake na polisi wanasema kuwa Islam anayefanya kazi katika Shirika la ndege la Emirates alimfanyia unyama mke wake huyo anayeitwa Hawa Akther Jui, mwenye miaka 21 , akamfunga midomo yake kwa matambara na kisha kuvikata kabisa vidole vyake vitano.Kwa mujibu wa taarifa ilichopishwa kwenye mtandao wa BBC (http://www.bbc.co.uk/news/world-asia-16201961 ) madaktari wamesema kuwa madaktari wamesema kuwa hawawezi tena kuvirejesha vidole hivyo na kwa maana hiyo binti huyo ataishi bila kuwa na vidole vitano vya mkono kwa maisha yake yote.
Narsingdi aliiambia BBC kuwa “ baada ya kurejea hapa Bangladesh alitaka kufanya mazungumzo na mimi lakini ghafla akafunga matambara machoni na kunibana vidole vyangu, akaniziba mdomo na kusema anataka kunipa zawadi nzuri ya kupendeza , lakini badala yae alinikata vidole vyangu”. Binti huyo anasema kuwa mume wake si mtu aliyeelimika vyema na ndio maana hakutka yeye ajiunga na masomo. Kwasasa amekata shauri la kuachana kabisa na mume wake.

0 comments: