Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, December 16, 2011

Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja amebakia na uhai wake baada ya kurushwa kwa makusudi kutoka ghorofa ya 10 na baba yake katika eneo la viunga vya jiji la Tokyo jana alhamisi.Tukio hilo limetokea saa tatu asubuhi hiyo jana huko Kiba na polisi wamemkamata kijana mmoja mwenye miaka 37 ambaye ni baba wa mtoto huyo kwa kumuhusisjha na tukio hilo baya la kikatili. Baba huyo alijitaja jina lake mbele ya waandishi wa habari kuwa ni Shingo Hashimoto.
Alinukuliwa akisema na kunukuliwa na Shirika la Kyodo News la hapa Japani kuwa “Nilijaribu kumuua mtoto wangu wa kiume , nilimkaba kwa mikono yangu na kisha nikamrusha chini, kutoka dirisha la chumba ninacholala
Polisi wamesema kuwa kijana huyo alikutwa na majeraha machache usoni nay eye mwenyewe Hashimoto ndiye aliyewaita polisi baada ya kufanya tukio hilo. Familia ya Hashimoto iliwaambia Polisi kuwa , mtoto wao alikuwa na msongo wa mawazo kutokana na kukosa ajira. Kijana huyo alikuwa akiishi yeye na mtoto wake huyo wa kiume baada ya mkewe mwenye miaka 38 na mtoto wake mwingine wa miaka minne kwenda matembezini. Bado jiihada za kuokoa maisha yake zinaendelea.

0 comments: