Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Wednesday, December 15, 2010

DAISO INDUSTRIES CO. LTD ni moja ya makampuni makubwa ya kibiashara nchini Japani yanayouza bidhaa zake kwa bei inayofanana. Kila kitu unachokiona dukani bei yake ni yeni mia moja na yeni tano ya kodi ambayo ni sawa na Shilingi za kitanzania 1,700 hivi. Kampuni hii ina maduka aina ya super market yapatayo 2500 nchini Japani na mengine zaidi ya 550 katika nchi mbalimbali duniani zikiwemo Marekani na ujerumani na nchi nyingi barani Ulaya na duka moja jingine kubwa lipo Ushelisheli barani Afrika. Raisi wa kampuni hii ni Bw. Hirotake Yano ambaye pia ndiye mmiliki wa kampuni hii. Nilibahatika kukutana naye (kama inavyoonekana pichani )katika pilikapilika za hapa na pale, hapa ni ofisini mwake. Ni mtu mkarimu na asiye na makuu.

0 comments: