Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, February 28, 2011

Posted by BM. on Monday, February 28, 2011

Mwanamume mmoja mkazi wa Warabi mkoani Saitama, amehukumiwa kwenda jela miaka mitano juzi Ijumaa na mke wake amehukumiwa kwenda jela miaka minne na usu kufuatia kifo cha mtoto wao wa kiume kilichotokea mwaka 2008 kutokana na ugonjwa wa kwashakoo.

Wanandoa hao Masami Shindo(47), na mkewe Sanae, (37) walikabiliwa na tuhuma za kuzembea kumpa lishe mtoto wao wa kiume na mahitaji ya kitiba kuanzia mwaka 2007 mwezi desemba wakati mtoto huyo akiwa na miaka minne hadi pale alipofariki dunia mwaka 2008 kutokana na kushikwa na na ugonjwa wa “Acute encephalopathy” , kwa kiswahili ‘ enkefalopathi sugu”.

Kulingana na taarifa ya polisi mvulana huyo mdogo alikuwa na uzito wa kilo 10 wakati anapoteza maisha. Polisi wamesema kuwa Shindo alikanusha kuwa mzembe katika kumlea mtoto wao akisema kuwa alikuwa akimpa chakula vizuri. Wanandoa hao wana watoto wawili mkubwa ana miaka kumi na kutokana na vifungo walivyopata wazazi wake mtoto huyo amepelekwa kwenye kituo cha kulelea watoto hadi pale wazazi wake watakapomaliza vifungo vyao.
Hali ya utapiamlo kwa watoto ni tatizo kubwa katika nchi hasa zinazoendelea....Picha hiyo ya mama anayenyonyesha imepigwa Kambodia katika familia yenye maisha duni...mtoto anataka kunyonya, maziwa hakuna..Ila hili la japani lipo 'tofauti kidogo 'Jaji kasema.

Posted by BM. on Monday, February 28, 2011

Idadi ya ‘ ndoa bandia' zinazowahusisha raia wa kigeni ambazo zimefichuliwa na jeshi la Polisi kote nchini Japani kwa mwaka 2010 kuwa zilifikia 153 ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.2 ikilinganishwa na mwaka uliopita. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Shirika la Taifa la Polisi hapa Japani.

Polisi walichukua hatua malimbali ikiwa ni pamoja na kuuliza maswali, kukamata na kupeleka nyaraka kwa waendesha mashitaka dhidi ya watu 471 wakihusishwa na tuhuma hizo. Shirika hilo limesema kuwa Polisi wanafuatilia miendendo ya ndoa hizo ‘bandia ‘ zenye malengo mbalimbali kama vile kutengeneza mazingira ya kufanya uhalifu.Shirika hilo limesema kuwa baadhi ya raia wa kigeni walijihusisha na vitendo vya jinai baada ya kupata hati za vya ukaazi kwa hatua yao ya kufunga ndoa za raia wajapani huku vikundi vya kihalifu vikipata fedha kutokana nandoa hizi za kupanga.

Source: http://www.japantoday.com/category/crime/view/no-of-fake-marriage-cases-involving-foreigners-surges-in-2010

Posted by BM. on Sunday, February 27, 2011

Fally Ipupa maarufu kwa jina la Di Caprio alizaliwa katika jiji la , akiwa Kinshasa katika familia ya mzee Ipupa Ebombo na mama Bolotuli Mbo mwaka 1977.


Alianza muziki tangu akiwa mdogo akiwa anaimbia bendi mbalimbali ambazo hazina majina huko DRC lakini jina lake liliibuka kwa kasi pale alipofanikiwa kuwa muimbaji wa kutumaini wa katika bendi ya Quartin Latin chini ya mmliki wake Koffi.

Fally alikuwa muimbaji wa kofii kutoka mwaka 1999 aliweza kufanya kazi kadhaa alipokuwa katika kundi la Quartin Latin ukiwemo wimbo wa Pharmacien katika album ya Monde arabe, aliweza pia kutunga wimbo wa Ko Ko Ko katika album ya (Affaire d'etat) pamoja na Eternellement (kwenye Force de frappe). Fally anasema yeye anavutiwa sana na mashairi ya Koffi na Papa Wemba kutokana na sauti yake lakini pia JB Mpyana Mpiana na Werrasone ni miongoni mwa wanamuziki anaowapenda.

Mwanamuziki huyu ana staili yake ya kuimba muda mrefu na kuacha muziki wa vyombo vitupu kiduchu tu…lakini staili hiyo haiwachoshi wapenzi wake kutokana na uwezo wake mkubwa wa kutunga mashairi Wale wanaojua kilingana hushikwa vilivyo na mashairi hayo na wale wasiojua lugha hiyo huvutiwa na mirindimo ya vyombo na sauti ya hisia kali aliyo nayo mwanamuziki huyu.
Ngoja nijaribu kukupa tafsiri ya wimbo huu subra! hii ni tafsiri yangu , pamoja na mapungufu yake unaweza kupata picha anachoisema!

Anaanza Ipupa; "Lakini tunakwenda kusubiria wapi?
Subiri….”Wako wapi sasa wale waliokuwa wakisema kuwa kitu mapenzi hakipo kabisa, Sasa hayo unaweza kuyaita nini?Kitu gani kimenipata, unaona nimekutana na wewe na moyo wangu ukatingishika!
Nimekua nikiwa mtu mwenye haya nyingi hata wazazi wangu wakitumai kuwa nitakuwa Kasisi siku moja ,wewe umeubadilisha mpango mzima wa maisha yangu,
Lepe zito la mapenzi limenizingira hadi katika nywele kichwani mwangu, unaweza kuwa na wasiwasi juu ya chochote lakini si wasiwasi juu ya mapenzi niliyonayo kwako. Mapenzi yameniweka katika hali ya kustaajabisha , kama vile kuangusha kilio bila ya kupigwa,
Chorus: Ni kwa umbali gani, mapenzi yako yamenisukumuma kwenye kaburi langu, ona nywele zangu za mvi zimeanza kurudia weusi wake tangu ulipoanza kunipenda!
Mtu anaposubiri boti huenda gatini,
Mtu anaposubiri ndege huenda Airport,
mtu anaposubiri treni huenda stesheni ya treni,
lakini pale mtu anaposubiri mapenzi anatakiwa aende wapi?
Si Ulianiambia nisubiri eti kwasababu mapenzi yanasubiwa…kweli!
…Nashangaa kama hilo bunge lililo katika moyo wako tayari limekwishaitisha mkutano kujadili suala letu , wewe Josee Mapwata…”
Hebu fuatilia mdundo na maneno ya Fally Ikupa kwa kubofya hapo!...

Posted by BM. on Sunday, February 27, 2011

Jiji la Ueno lipo katika viunga vya Tokyo. Hapo kuna mtaa mmoja maarufu sana wa kibiashara nauita 'mtaa wa sikukuu'. Hapo kuna mishemishe za kutosha .

lakini upekee wa mtaa huu ni uuzaji wao wa vyakula vya baharini, samaki, pweza, kombe , konokono bahari , sato'sijui wa Mwanza?'
Hata matunda ya vijiti, mapapai, mananasi na stroberi yanapatikana. Ooh nimekumbuka wanauza ukwaju na urojo na mishikaki ya siki kama kwetu Forodhani, Unguja. hebu tembelea mtaa huo kwa njia ya picha!


Posted by BM. on Sunday, February 27, 2011

Posted by BM. on Sunday, February 27, 2011


Posted by BM. on Sunday, February 27, 2011

Mahakama moja katika Mkoa wa Saitama hapa Japani imewahukumu wanaume wawili miaka miwili jela kila mmoja kwa kushindwa kumkataza rafiki yao aliyekuwa amekunywa pombe wakiwa pamoja naye kuacha kuendesha gari , hali ambayo ilisababisha kupata ajali barabarani.


Tukio hilo ni la mwaka 2008 lakini hukumu imetolewa juzi huku wakili wao akisema kuwa ni mara ya kwanza kwa mahakama hiyo kuwakumu watu kwa kushindwa ‘kutimiza wajibu wao wa kumkataza mtu aliyekunywa pombe kuacha kuendesha gari.
Uamuzi huo wa kuwafunga watu hao umefikiwa na jopo la majaji wazoefu na majaji watatu wa kiraia (Kama wazee wa baraza kule Tanzania) . Jaji aliyeongoza jopo hilo Makoto Tamura amesema kuwa anamuadhibu Isao Oshima mwenye umri wa miaka 48, na Junichi Sekiguchi (46) kwa kumruhusu mwenzao kushika usukani bada ya kunywa pombe.

Katika siku hiyo , gari la watu hao liligongana na jingine lililokuwa likija mbele yao huko Kumagaya mkoa wa Saitama na kuwaua wapenzi wawili . Dereva mwenyewe alihukumiwa kwenda jela miaka 16.

Timu ya mawakili inayotoa utetezi imesema kuwa haijafurahishwa na hukumu hiyo na familia hiyo inataka kukata rufaa.
(Tafadhali..picha hizo hazina uhusiano wa moja kwa moja na habari hii ni mfano wake)

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Fuatilia mazungumzo haya ya Larry King na Muammar Gadaffi , unaweza kuanza kumjua Gaddaffi huyu anayepata misukosuko hii leo.

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Imoto Ayako Ni maarufu sana nchini Japani hususan miongoni mwa vijana na watu wa rika la kati na wafuatiliaji wa habari. Huonekana katika vipindi va televisheni vya burudani. Ni nguli katika ubunifu , ujasiri na uthubutu. Amesafiri kila pembe ya dunia akishiriki katika matukio mbalimbali ya kufurahisha na ya kutisha na hata kuhatarisha maisha yake huku akirekodiwa na baadaye vipindi hivyo hurushwa na kituo kimoja cha televisheni hapa Japani. Wajapani na wageni wa marika yote hapa japani wanamjua mdada huyu kwa pilika pilika zake.


Kwa sasa binti huyu Imoto Ayako ana miaka 23 na mara zote ukikutana naye au akiwa ndani ya kipindi huonyesha ucheshi na furaha . Vazi lake linalomtambulisha ni sare ya shule na usoni akiwa amejipaka wanja mzito. Bila shaka hii ni mbinu yake ya kujitambulisha.
Hapa Japani kuna kituo kimoja cha televisheni kinarusha kipindi kinachoitwa “Sekaino hatemade ittekyuu”. Hapo yeye ndiye ‘stelingi’ watu wanaangalia kazi yake na baadaye kuzjadili kwa mshangao na furaha kubwa.Itkumbukwa binti huyu ameshapanda hadi katika kilele cha Mlima Kilimanjaro mwaka 2009 , na kuna kipindi kilionyeshwa akiwa anacheza na mamba katika mto Nile na wakati fulani akifukuzwa na chu, achilia mbali kuruka na parachuti baada ya mafunzo ya wiki moja.

Katika kuonyesha kuwa anathubutu mambo mengi mwezi August mwaka jana alikimbia takriban kilometa 126.5 akikimbia bila kupumzika kwa saa 26 na dakika tano katika mbio za kujitolea ambapo televisheni moja inayotangaza kwa saa 24 hapa Japani ilikua ikikusanya fedha na kutoa habari zinazohusu masuala ya Kijamii , mazingira na huduma za majanga. Ameandika vitabu kadhaa vinavyouzwa kote duniani vikielezea mwenendo wa maisha yake. Unaweza kumuangalia Imoto Ayako katika clips mbalimbali za You tube kwa sasa anza na hii hapa!Kuhusu mbio hizo zilivyokuwa unaweza kubofya:http://www.japan-zone.com/news/2009/08/31/a_triple_marathon_weekend.shtml
Take 5 mdogo Imoto!

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011


Ilikuwa kiroja katika mitaa ya Biafra kinondoni hivi karibuni alipojitokeza mdada mmoja 'kwa raha zake' akipita na kimini utata karibu na kituo cha basi huku watu wa malika tofauti wasiamini wanachokiona....eeeh eeh!
Akimama wa mtaa huo walimchangia pesa akodi taix na badala yake akanunua kiroba alichokishika mkononi. Uhuru sawa , .com sawa au ndio uzungu ?
Tunakokwenda kazi kweli kweli!. (Picha na mtandao wa Pwani-raha).


Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Mtoto kutoka kabila la wahimba nchini Namibia!

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Umeshaliona kama hili au kulipanda?

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Posted by BM. on Tuesday, February 22, 2011

Posted by BM. on Sunday, February 20, 2011

Polisi wa kutuliza ghasia nchini Bahrain wamewatawanya waandamanaji kati uwanja maarufu ulio katikati ya nchi hiyo na hivyo kuwalazimisha kurejea eneo ambalo awali walikuwa

.Walifika hapo wakakutana na polisi na baada ya nusu saa hivi Polisi wakawamwagia risasi na kuwauwa waandamanaji kadhaa hapo hapo kama unavyoweza kuona kwenye video hiyo ilichukuliwa na mwandishi wa habari wa Shirika la Aljazeera la Qatar.

Waandamanaji hao walikuwa wakipiga mayowe huku wakiibusu ardhi huku wakichukua picha na magari ya polisi yanayokadiriwa kufikia 60 yakliwazunguka.Hospitali maarufu ya Salmaniya imekuwa ikipokea majerhi na maiti za waandamanaji.Inasemekana kulikuwa na maagizo ya familia ya kifalme inayoongozwa na mfalme mwenyewe Hamadi bin Issa bi Khalifa kuhakikisha mitaani hakuna watu na Polisi walitekeleza amri hiyo bila kujali maisha ya watu.

Mamia wa akinamama waliovaa abayas nyeusi ( Baibui na hijabu) waliungana katika maandamano hayo yanayoitaka Serikali ya kifalme kuondoka na kuingia ya kidemokrasia.
Wasiwasi umetanda nchini humo , na kipandauso hicho kimezaa kwa viongozi wote katika nchi za kiarabu... (Taarifa na Aljazeera)

Posted by BM. on Sunday, February 20, 2011

Posted by BM. on Friday, February 18, 2011

Wakenya wanaonekana kuwa wanakunywa kiasi kikubwa cha pombe ikilinganishwa na nchi zote za Afrika mashariki ingawa Uganda ipo kileleni katika idadi ya wazalishaji wasio rasmi wa pombe .

Taarifa ya karibuni kabisa ya unywaji wa pombe iliyotolewa na Shirika la Afya Ulimwenguni-WHO na kuchapishwa na magazeti ya Kenya inabainisha kuwa takriban nusu ya wanywaji wa pombe nchini Kenya wanapendelea kunywa bia , wakati katika nchi za Uganda na jirani zao Tanzania wanapendelea zaidi pombe za kienyeji.

Takriban asilimia 90 ya wanyaji wa pombe katika maeneo ya mipaka wanapenda kunywa pombe za kuchachushwa kama vile waragi, muramba, tonto na nyinginezo zinazotengenezwa kienyeji.Msaidizi wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO , Dr. Ala Alwan ambaye anahusika na magonjwa ya kuambukiza na afya ya akili amesema kuwa nchi nyingi zimebaini madhara makubwa yanayotokana na matumizi ya kilevi kupindukia , hivyo kuna haja ya kuchukua hatua zaidi.Ripoti iliyoisifu Kenya kwa ulevi inabainisha kuwa takriban asilimia 17 ya wanafunzi wa kiume nchini humo na asilimia 12 ya wanafunzi wa kike walikutwa wakinywa pombe katika siku 30 za awali kabla ya kuanza rasmi kwa utafiti unaohusu unywaji wa pombe.

Hali hii pia imejitokeza katika nchi za Tanzania na Sychelles ambako asilimia 60 ya wanafunzi wa Sekondari, high schools, na vyuo vikuu wanakunwa pombe kwa viwango tofauti.Taarifa hiyo inasema kuwa mbali na imani iliyojengeka awali kuwa Wakenya si wanywaji sana wa pombe , lakini ukweli ni kuwa wale wanaokunywa , wengi wao huwapiga wake zaozaidi ya mara mbili kwa wiki, chanzo kikiwa pombe.Sijui inatupa picha gani watu wa Afrika Mashariki. Bila shaka ni kupanuka kwa soko la Kilevi na kuongezeka kwa ‘walevi’ katika eneo letu . au siyo!

Posted by BM. on Friday, February 18, 2011

Baada ya kusbiri kwa miaka mingi kuitwa baba Fulani hatimaye Ramajit Raghav amekuwa baba wa mtoto wa kiume kwa mara ya kwanza akiwa na miaka 94 na ushee hivi.
Ramajit anayeishi katika kijiji kimoja nchini India anayefanya kazi katika shamba la kabaila mmoja nchini India kwa miaka 22 alimuoa Bi. Shakuntala, akiwa mke wake wa pili takriban miaka 10 iliyopita , mke ambaye sasa anasemekana ana miaka 50.
Bi. Shakuntala alilazwa katika hospitali ya Serikali katika mji wa Kharkoda na akajifungua kwa njia salama kabisa mtoto wake wa kiume.


Wazazi hao waliojawa na furaha tele walimuita mtoto wao jina la Karamjit na baba yake huyu alisema kuwa ilikuwa zawadi kutoka kwa Mwezi Mungu, na amempata mtoto huyo akiwa n fahamu zake na akili timamu.

Alipoulizwa juu ya maisha ya mtoto huyo kwa kuzingatia ukweli kuwa yeye ni mzee wa miaka 94 , Mzee Rajamit alisema kuwa “ najua hakuna baya litakalotokea kwa mtoto wangu , Mye nitakufa tu ikiwa nyoka mweusi atanigonga na hiyo haitokei leo wala kesho”. Mzee huyo hakuishia hapo akasema “Nitembelee tena baada ya miaka 10 utanikuta kama unavyoniona hii leo”.
Kuzaliwa kwa mtoto huyu kunamfanya Ramajit kuvunja rekodi ya mzazi wa zamani aliye na umri mkubwa zaidi ambaye alipata mtoto akiwa na miaka 90 akiwa amepata mtoto wake wa 22 mwaka 2007 na huyu ni Nanu Ram Jogi, -
(Habari hizi ni kwa mujibu wa Shirika la habari la ATULA la huko India).

Posted by BM. on Friday, February 18, 2011

JIJI la Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana alhamisi limejikuta katika hali ya sintofahamu baada ya milipiko mikubwa ya mabomukutokea katika ghala namba tano la kutunzia silaha la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Gongolamboto, huku kukiwa na taarifa za watu 15 kufa na zaidi ya 60 kujeruhiwa. Nyumba nyumba kadhaa zikiteketea kwa moto baada ya kuangukiwa na mabomu.




Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk Hussein Mwinyi, alisema milipuko hiyo ilitokea ghala namba tano na kwamba, kilichokuwa kikifanyika ni kuzuia usienee sehemu nyingine.

Mwaka 2008 kulitokea mlipuko ghala la silaha kwenye kambi hiyo ya jeshi la Gongo la Mboto katika tukio ambalo vyombo vya usalama vilidai kuwa ulitokana na silaha hizo kupata joto kali.
Raisi jakaya Kikwete alitembelea eneo la tukio kujionea hali halisi na baadaye akaongea na waandishi wa habari..
Blogi ya MIRINDIMO inawapa pole wote waliofikwa na maafa haya , Mungu awape subra katika kipindi hiki kigumu wanachokabiliana nacho... (Picha kwa hisani kubwa ya Issa Michuzi Blog)

Posted by BM. on Thursday, February 17, 2011

ENTEBBE, Uganda (AFP) – Veteran President Yoweri Museveni on Wednesday predicted a landslide victory in polls this week, dismissing his main challenger's assertion that Uganda was ripe for an Egypt-style uprising."It will be a big win," Museveni, who has been in power for 25 years, told reporters at the presidential palace here ahead of Friday's election. "We shall win with a big majority."

Many commentators believe Friday's presidential election could be the closest since Museveni, a former guerrilla leader, grabbed power as head of the National Resistance Army in 1986.In 1996 polls, he took 75 percent of the vote, but his share dropped to 69 percent in 2001 and to 59 percent in the 2006 election.The campaign though has illustrated how he retains a formidable support base with tens of thousands of youths attending his final rally at an airstrip on the outskirts of Kampala on Wednesday afternoon.All those attending the rally, which included a concert by local musicians, had to undergo body checks, with Uganda having previously been targeted by Islamist bombers over the presence of its troops in Somalia.Observers say the opposition's best hope is to deprive Museveni of more than 50 percent of the vote, and then unite against the incumbent in a second round.

The most prominent of his seven challengers, Kizza Besigye, says Uganda has floundered under Museveni's rule and the opposition could ride a wave of revolt that has deposed despotic presidents in Cairo and Tunis.
Besigye's election posters around the capital Kampala promise "Change is Coming" but Museveni has dismissed comparisons with events in North Africa."We are not worried at all ... you just wait, you will see," Museveni said.
"There will be no Egypt-like revolution here ... Egypt is a different story. Tunisia is a different story."
Besigye said during the campaign that only rigging by the ruling party can deprive him of victory, and pledged to produce his own vote tally to challenge the official result, if necessary.Asked how he would react if Ugandans take to the streets to contest the poll results, Museveni said: "We just lock them up ... bundle them into jail and (bring them) to the courts."However, most analysts believe that Museveni, 67, will still secure enough votes to win another five-year term."By the end of these five years Uganda will be a middle-income country. I will not allow Besigye and others to mess up that plan," said Museveni before heading into the capital for a final campaign meeting.Besigye meanwhile held his last campaign rally on the campus of Makerere university. More than 10,000 enthusiastic supporters danced and screamed as they waited for his last speech of the campaign."I'm here to join and sing in one voice that change is coming," said 20-year-old Besigye supporter Jonathan Mukiibi. "Museveni has not provided anything for us."
Besigye ran against Museveni in 2001 and contested the results, but fled the country after a court awarded the election to his opponent. He returned to contest the 2006 election while at the same time fighting off rape and treason charges which were only dismissed after the polls had taken place. This time around, he has campaigned against Museveni without incident.


The president himself acknowledges that corruption, a key campaign issue, is rampant in the country. But he can point to a growing economy and future oil revenues, even if a third of Uganda's 33 million people live on less than one dollar a day. The incumbent's prospects have been further enhanced by two other key factors: the successful army offensive that pushed the feared Lord's Resistance Army rebels into neighbouring countries, and the fact that the opposition have failed to field a common candidate

Posted by BM. on Wednesday, February 16, 2011

Posted by BM. on Tuesday, February 15, 2011

Kumekucha ....barabara zimejaa barafu na mapaa kuna mabonge pia ya barafu.Usiku kucha mvua ya theluji ilidondoka lakini hali imetengamaa asubuhi...picha ya mapaa ya nyuma za majirani na mitaani katika viunga vya jiji la Tokyo...nimeshuhudia..



Posted by BM. on Tuesday, February 15, 2011

WASHINGTON –VALENTINE= Here's Michelle Obama's advice for couples this Valentine's Day: Laugh with your partner.
She says it's what she and President Barack Obama do, and it seems to be working. Their marriage, although tested throughout the years by his political ambitions — for the Illinois Senate, the U.S. Senate and later president — is going on 19 years.


"I think a lot of laughing," the first lady said recently at a White House luncheon with reporters who asked about the Obamas' union. "I think in our house we don't take ourselves too seriously, and laughter is the best form of unity, I think, in a marriage."So we still find ways to have fun together, and a lot of it is private and personal. But we keep each other smiling and that's good," she added.


It also helps that Obama is "very romantic.""He remembers dates, birthdays," Mrs. Obama said last week on "Live! With Regis and Kelly." "He doesn't forget a thing, even when I think he is. . I'll have a little attitude. I give him a little attitude, but he always comes through.""Got to keep the romance alive, even in the White House," she said.

As for Valentine's Day on Monday, the first lady said her husband would do right by giving her jewelry."You can't go wrong," she said. But Mrs. Obama also said they don't fuss too much over the day that's about celebrating love and affection between couples.Last year, the Obamas spent Valentine's Day at the Camp David presidential retreat in Maryland.In 2009, their first year in the White House, they went home to Chicago and enjoyed a quiet dinner at Table 52, a traditional Southern restaurant owned by Art Smith, the former chef of Obama pal Oprah Winfrey.How will they celebrate this year? By staying in, apparently. The White House announced a "travel lid" Monday afternoon, which meant Obama had no plans to leave the grounds again for the day. He visited a Baltimore middle school in the morning.


"We don't make a big deal out of Valentine's Day because my birthday was the 17th (of January)," she told Regis Philbin and Kelly Ripa. She noted, too, that Christmas was just a few weeks before that."So by Feb. 14, we're kind of tired," Mrs. Obama said.For her 47th birthday last month, the Obamas dined at The Source, celebrity chef Wolfgang Puck's restaurant at the Newseum in Washington.

Posted by BM. on Sunday, February 13, 2011

Moja ya adhabu zilizokuwa zikikera sana nyati zilee ni pamoja na hii , kushika masikio, kuruka kichura na makonzi...sijui kama siku hizi zinaendelea lakini zilikuwa zikiogopwa sana miaka ile...siju kama zilisaidia!

Posted by BM. on Sunday, February 13, 2011

Raisi Mteule wa Sudani Kusini Mh. Salva Kiir Mayardit

Posted by BM. on Sunday, February 13, 2011


Posted by BM. on Saturday, February 12, 2011

Maeneo mengi ya Tokyo jana Ijumaa yaligubikwa na barafu ...na hali ya hewa ilikuwa kibaridi kikali kilichofikia nyuzi joto MOJA hadi SIFURI...

. Kaskazini na kusini mwa Japani kwa sasa barafu inadondoka kwa wingi lakini kwa Tookyo wiki hii ndio ilianza na jana ilikuwa ndio siku nzima...


Mtaani kwetu hapo...