Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, December 19, 2010

Hili ni behewa la treni ambalo ni maalum hapa Japani ambalo limetengwa kwa ajili ya wanawake tu katika nyakati fulani fulani hasa inapokuwa kuna misongamano....asubuhi, usiku na siku za sikukuu..

Jioniy ya jana wakati ambapo ilikuwa ruhsa ya kupanda humo watu wote bila kujali jinsia zao..ndipo nikakutana na familia moja ...Mtoto wa kike wa kizungu wa miaka saba hivi alimuuliza mama yake "Kwanini wanawake tu...kwanini baba haruhusiwi kupanda humu"?.
Wazazi wake walitumia muda mrefu kufafanua ...na mara kadhaa alikuwa akirudia swali lake ...kwanini baba na kaka(mdogo wake wa kiume aliyekuwepo) asipande?. Nadhani alielewa...nilifurahia mjadala ule , hususan udadisi wa watoto.

0 comments: