Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, April 20, 2009

Hii ni hatari! Kuna tukio la kusikitisha limetokea hivi karibuni huko kaskazini mwa Texas , nchini Marekani . Mwanamama mmoja alikuwa katika boti jumapili moja , akachukua baadhi ya soda za kopo za Cocacola na kuweka kwenye friji iliyopo katika boti hiyo huku akila wikiend na baadaye akazinywa kwa raha zake.
Siku iliyofuata ya jumatatu alipelekwa hospitalini na kuwekwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi na siku ya jumatano akafariki dunia. Uchunguzi wa kitiba umeonyesha kuwa alikufa kutokana na ugonjwa wa Leptospirosis. Hii ilitokana na kunywa ile soda bila kutumia glasi na uchunguzi umeonyesha kuwa Alikula na mkojo wa panya uliogandiana juu ya mdomo wa kopo uliomsababishia ugonjwa huo wa Leptospirosis ambao unaua kama umeme. Mkojo wa panya una sumu inayoua na ndio maana inashauriwa kusafisha sehemu ya juu ya vyakula na vinywaji vya makopo kabla ya kula au kunywa. Makopo haya hujazwa kwenye maghala na kupelekwa madukani bila kusafishwa. Utafiti uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa makopo ya soda yana mabaki ya sumu yaliyo hatari kuliko vilivyo vyoo vinavyotumika na watu wengi ambavyo vina germs na bacteria wengi tu. Kuwa mwangalifu…

0 comments: