Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, May 29, 2009

Picha hiyo juu inaonyesha wapenzi hao walivyokuwa miaka 81 iliyopita na picha ya chini hivi sasa. Jumanne wiki hii walisherehea miaka 81 wakiwa ndani ya ndoa thabiti na kuvunja rekodi nchini Uingereza kwa kukaa ndani ya ndoa kwa muda mrefu.
Mzee Frank na mkewe Anita Milford wote wakiwa na miaka 101 wanaishi pamoja katika nyumba ya kulelea wazee huko Plymouth, nchini Uingereza na rekodi inaonyesha walioana tarehe 26, Mei , 1928. Mzee Frank alistaafu miaka 41 iliyopita na bado wanaikumbuka vita ya pili ya dunia ya mwaka 1945 kuwa walinusurika mara mbili kufa kwa mabomu pale bomu moja lilipoanguka karibu ya nyumba yao. Wapenzi hao wana watoto wawili , wajukuu watano na vitukuu saba. Mtoto wao mkubwa ambaye pia anaitwa Frank kama baba yake ana miaka 74. Aisee bahati kubwa ! hebu nawe jiulize ulikaa miaka au miezi mingapi na mwenza wako wa MWISHO kabla hamjatibuana ?…....................ishakuwa tabu!

Frank na Anita

0 comments: