Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, June 29, 2009


Kifo cha ghafla cha Prof. Haroub Othman, kimewashitua watu wengi nchini baada ya kufariki ghafla asubuhi ya kuamkia jana jumapili akiwa usingizini. Kimewashitua wengi kwa sababu usiku wa kuamkia jana hiyo alikuwa miongoni mwa mamia ya watu waliohudhuria tamasha la filamu na kabla ya hapo alikuwa mgeni rasmi aliyesoma hotuba wakati wa kuzindua kitabu huko huko Zanzibar. Marehemu alikuwa mtetea haki za binadamu na mkosoaji mkubwa wa masuala ya kisiasa, hivyo kifo chake kimeacha maswali mengi kuliko majibu. Wakati akiwa katika Tamasha la filamu, Prof alionekana mwenye afya na mwenye furaha wakati wote, hasa wakati msanii Mrisho Mpoto alipokuwa akituimbuiza kwenye uzinduzi huo na alionekana akisalimiana na Profesa mwenzie wa Kenya.

1 comments:

mumyhery said...

inna lilah wainna illaiyhi ranjuun