Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Monday, June 29, 2009


Raisi ya wa zamani wa Zambia Fredrick Chiluba amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashitaka ya kutumia vibaya fedha za umma zinazofikia takriban Paunti za kiingereza laki 5 na ushee kinyume na sheria kati ya mwaka 1991 hadi mwaka 2001 alipokuwa madarakani .Kesi hiyo ilisimama mwaka 2003 kutokana na sababu za kisheria na matatizo ya afya ya raisi huyo mstaafu. Chiluba mwenye miaka 64 alionekana katika Korti ya Lusaka akiwa na majonzi makubwa.Moja ya vizibiti muhimu katika kesi hiyo ni viatu vyake vinavyotajwa kuwa vina thamani kubwa sana .

. Mahakama iliombwa kumruhusu kusikiliza kesi akiwa nyumbani kwake kwanjia ya video lakini ilikataa ikasema lazima akalie mabechi ya mahakama. Mke wake anaonekana picha ya hapo juu akiwa katikati yao hivi sasa anatumikia kifungo baada ya kupatikana na hatia ya ubadhilifu wa fedha.

0 comments: