Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, November 10, 2009

Labda hili!
Kijana mmoja aliyekuwa anatafuta kazi alifanikiwa kupata kazi katika zoo ya wanyama. Kijana huyo ilimbidi afanye hiyo kazi japo ni ngumu lakini alikuwa hana jinsi. Kazi hiyo ilimtaka kijana huyo kuvaa ngozi ya sokwe na kurukaruka kwenye banda la sokwe ambae alifariki ghafla, kwa kuwa watalii wengi walimpenda huyo sokwe, ilibidi mmiliki wa zoo amfundishe huyo kijana staili zote ambazo Yule sokwe alikuwa akiruka. Kijana alifanikiwa mbinu hizo na kuanza kazi mara moja huku watalii wakimiminika kuona sokwe wao karudi. Siku moja kijana huyo katika kurukaruka kwake kwa sifa alijikuta amedondoka kwenye banda la simba. Simba huyo alimkimbilia huyo kijana na kumuinamia huku watalii wakishangaa kuona nini kitatokea. Kijana alianua mdomo kwa kutaka kupiga kelele mana alishaona maisha yake yako hatarini lakini cha ajabu alisikia simba akimnong'oneza ''Acha kelele tutafukuzwa kazi''Kumbe ..

0 comments: