Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Thursday, May 13, 2010

Jumuia ya watanzania wanaoishi Japani TANZANITE inawataarifu kuwa kuwa imeandaa tafrija ndogo ya Kumkaribisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Japani Mh. Salome Sijaona sambamba na kumuaga Ofisa Ubalozi mwandamizi, Bw Elibariki Maleko ambaye anatarajia kurejea nyumbani Tanzania hivi karibuni baada ya kumaliza mkataba wake wa kikazi hapa Japani.
Jumuia hiyo imetoa taarifa za kina juu ya hafla hiyo kuwa; itafanyika Siku ya Jumapili, tarehe 30 Mei 2010.
Muda: Kuanzia saa kumi jioni mpaka saa mbili usiku (16:00 - 20:00).
Mahali: Ukumbi wa Tsuruma.Taarifa ya jinsi ya kufika kwenye ukumbi itatolewa baadaye.
Ili kurahisisha shughuli za maandalizi, kama chakula na vinywaji, tunaomba wale wote watakaotaka kuhudhuria kuandikisha majina yao kwa kwa viongozi wafutao:

1. Abby senkoro: mail: ewsenkoro@yahoo.com, Simu: 090-9801-4433
2. Juma Kipya: 080-3414-4460
3. Upendo Mwimbage: 080-1326-9700
4. Mariam Yazawa: 090-4422-8555
5. Yasir Kiluke: 090-4203-3340
6. Bagilo Jumbe: 090-1733-7447
7. Amani Paul: mail: amani.paul@gmail.com, simu:080-4200-0684

Siku ya mwisho ya kujiandikisha ni tarehe 22/5/2010. Pia tunaomba kusisitiza kuwa wale ambao hawatajiandikisha majina yao hawataruhusiwa kuingia ukumbini siku ya tafrija. Na wale watakaohudhuria wazingatie muda kwasababu ukumbi umekodiwa mwisho saa 2 kamili usiku hivyo tunawaomba wafike kwa muda unaotakiwa.

Balozi wa TZ hapa JP Mh.Sijaona alipowasili hapa Japani na kupokewa na Bw. Maleko , Afisa mwandamizi wa Ubalozi huo hapa Tokyo.

1 comments:

Anonymous said...

Asanteni ndugu zetu kwa ukarimu wenu ufaao na tunamkaribisha sana nyumbani kaka yetu Bariki Maleko.