Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, November 14, 2010

Kiongozi wa upinzani nchini Myanmar, Aung San Suu Kyi ameachiwa huru leo na uongozi wa kijeshi wa nchi hiyo. Uongozi wa kijeshi nchini Myanmar umemuachia huru kiongozi wa upinzani nchini humo, Aung San Suu Kyi. Magari maalum leo yaliwasili katika nyumba ya kiongozi huyo iliyoko pembezoni mwa ziwa na polisi waliondoa vizuizi pamoja na senyenge.
Katika kipindi chake cha kukaa Kizuzini Suu alilazimika kuzunguka ndani ya Seng'enge na kukaa chini ya mti nje ya nyumba yake hadi wakubwa walipoamua kumtoa nje kwa shinikizo la jumuia ya kimataifa.


Suu Kyi aliusalimia umati wa wafuasi wake wapatao 1,000 ambao walikuwa wamekusanyika katika lango la kuingilia kwenye nyumba hiyo. Mshindi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobel, ametumikia kifungo cha nyumbani kwa takriban miaka 21. Akiwa katika hali ya kujiamini Bi. Suu aliongea na waandishi wa habari;
Haijajulikana bado nini anakipanga kukifanya kiongozi wa kijeshi nchini humo Generali Than shwe (Pichani )kwa mara nyingine tena , ambaye kila kukicha humzulia jambo Suu na kumuweka kizuizini.



0 comments: