Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, November 30, 2010

Tetemeko lenye ukubwa wa 6.9 kwa kipimo cha richa limetikisa pwani ya kusini ya jiji la Tokyo nasi katika jengo la utangazaji limetutikisa kwa muda wakati tukiendelea kurusha matangazo.Majengo yalitikiswa katikati ya Tokyo lakini kutokana na kuwepo kwa teknolojia ilionekana kama vile yakiyumba hivi.

Hakuna majeruhi wala uharibifu ulioripotiwa hadi sasa na idara ya utabiri wa hali ya hewa imesema kuwa hakuna tisho la kuwepo kwa mawimbi ya tsunami kwahiyo hali inatarajiwa kuwa shwari.Mtetemo huo ulitokea saa sita na dakika 25 mchana huku kitovu cha tetemeko hicho kikitajwa kuwa kilikuwa karibu na visiwa vya Ogasawara takriban kilometa 800 na lilitokea kilometa 480 chini ya ardhi . Ingawa vipimo vya idara ya hali ya hewa ya Japani inasema kuwa tetemeko lilikuwa na ukubwa wa 6.9 , ile ya Marekani ilisema ilikuwa na ukubwa wa 6.6.

0 comments: