Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, January 14, 2011

Mtu mmoja mwenye miaka 52 amekamatwa jana jumatano huko Kobe hapa Nchini Japani kwa kumuandikia ujumbe binti mmoja mwanafunzi amtumie picha zake akiwa uchi mtupu , akituhumiwa kuvunja sheria inayokataza matumizi ovyo ya picha chafu.
Mtuhumiwa huyo amefahamika kwa jina la Nobuhito Mizohata, aliyetuhumiwa kutumia picha bandia inayomuonyesha kama kijana akiwa katika eneo la miadi kwa lengo la kumshawishi binti wa miaka 16 anayeishi huko Nagoya.

Taarifa za kipolisi zimebainisha kuwa ombi la Mizohata lilifanikiwa na alipokea picha za binti huyu akiwa uchi aliyoichukua kwa njia ya kamera ya mwezi septemba mwaka jana simu yake ya mkononi .
Polisi walimnukuu Mizohata akisema kuwa “Nataka mabinti wadogo na nilitaka picha wakiwa tupu kutoka kwao “Baada ya kuangalia kile alichokifanya Mizohata katika komputa yake , Pilisi waligundua picha nyingi mbalimbali na ndipo walipomuhoji ni mara nyingi kiasi gani amekuwa akifanya hivyo kabla hajaingia kwenye mtego wa polisi

0 comments: