Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Wednesday, July 20, 2011

Jana tulirekodi kipindi chetu cha 'Sauti ya Antyango' Katika Idhaa ya Kiswahili ya Redio Japani hapa Tokyo nikiwa na mtayarishaji mwenzangu msanii maarufu wa ngoma za kijadi za Afrika Mashariki hususan Kenya ya Nyatiti Bi. Erico Mukoyama maarufu Anyango! ambapo tuliwachambua wanamuziki kadhaa akiwemo Sakaki Mango, huyu anacheza chombo cha asili cha kigogo cha limba...



Baadaye nilifanya mazungumzo na mdada wa Kifaransa..Bi Amina Abdala...yeye ni mzaliwa wa Lamu kule Kenya lakini amekulia Ufaransa na sasa ni director wa Anyango Foundation huko Ufaransa , ambayo inaratibu ziara za Anyango barani Ulaya , kufundisha muziki wa kijadi huko pamoja na kusambaza CDs.



Recording hiyo ilishuhudiwa na Mkuu wa Idhaa za Kigeni wa NHK , Bi, yuko Asano na wafanyakazi wa Idhaa ya Kiswahili...


Amina alipata fursa ya kunionyesha kazi anazofanya huko Ufaransa alizozihifadh kwenye komputa yake,...
Ukipenda kumuona Mjapani anayecheza ngoma za Kigogo Sakaki Mango bofya hapo chini.....

1 comments:

Amina Abdala said...

Asante sana na matangazo. Nilifurahiya sana kukutana na wewe.
Salama