Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Sunday, July 17, 2011

Kwenye mtandao mmoja wa Kibiashara, bidhaa mbili mpya zimetangazwa. Moja ni Mo na nyingine aina mpya ya gari ya Mazda. Nakuletea picha zake...


Mo:Ben ni chombo kidogo cha nyumbani ambacho kimejengewa kikanza (Heater) ambacho kinaweza kupasha moto chakula na kuurejesha ujoto uliokuwepo awali. Ni kiasi cha ku-tyuni tu joto linaanza kusambaa kunako kikanza. Vifaa vya namna hii viko vingi Japani lakini kinachofanyika ni kuvipa muundo mpya kila kukicha..

Aina mpya ya gari ‘Mazda’ imejitokeza kuingia kwa vishindo katika soko la magari ya kifahari nchini Japani na kufahamika sana kwa jina la “Kiyora”. Kwa kijapani Kiyora ina maanisha ‘Safi na halisi’ ikiwa na silinda nne , injini inayotoa kiwango kidogo cha kaboni na inatumia mafuta machache. Umbile lake ni la kipekee na linavutia. Unaweza kumuona dereva akiwa ndani ya gari na maji ynayotiririka kuleta ubaridi katika gari…

0 comments: