Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Tuesday, November 08, 2011

Wanasayansi nchini Japani wamevumbua teknolojia ya kutengeneza bidhaa za plastiki kwa kutumia mwani …ule usioliwa ambao hutanda baharini .
Hatua hiyo itawezesha mabaki hayo ya plastiki kuoza ikiachwa ardhini. Hatua hiyo imekwenda mbali zaidi ambapo sasa wapo kwenye hatua za mwisho mwisho za majaribio ya kimaabara ambapo mwani huo utatengeneza nyuzi za kushonea miili ya binaadamu (Surgical threads) ambazo zitaoza sambamba na kukauka kwa kidonda.

Mwani umekuwa ukitumika pwani ya Afrika Mashariki kama mlo aghalab zaidi kwa wageni lakini hapa Japani hutumika sana katika maakuli, mbolea mashambani na sasa unataka kuumika katika hatua hii mpya.. Unaweza kufuatilia makala hii ya kusisimua kwa kusikiliza kipindi cha cheche za teknolojia kupitia mtandao huu; http://www3.nhk.or.jp/nhkworld/swahili/top/index.html Ukifika ukurasa huo angalia vipindi vya Jumanne, Nov,8 , bofya hapo na anza kusikiliza.

0 comments: