Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, November 05, 2011

Wakazi wa jiji la Bangkok , nchini Thailand bado wako kwenye hekaheka za mafuriko baada ya maji kuvamia makazi yao.Waziri mkuu wa nchi hiyo Bi.Yingluck Shinawatra (Pichani mwenye blauz nyeupe)amewahakikishia wakazi wa mji mkuu wa nchi hiyo Bangkok kuwa serikali inakabiliana na mafuriko ambayo yameuwa watu takribani mia mbili themanini na tisa na kusababisha hasara ya takribani dola bilioni tatu .
Waziri Mkuu Bi.Yingluck Shinawatra alitumia ndege ya jeshi kukagua mafuriko hayo na baadaye akafika kwenye eneo hilo na kuwafariji waathirika (Moja ya picha akiwapa mikono)

Mji wa Bangkok ambao unapatikana mita mbili pekee kutoka usawa wa bahari unaendelea kuwa hatarini kutokana na kuongezeka kwa maji kutoka vyanzo vya maji Kaskazini mwa mji huo ambavyo vinasababisha kufurika kwa mto Chao Phraya.Baadhi ya wananchi walionekana wakihamisha mali zao na kuzipeleka katika maeneo ambayo hayajaathiriwa.Huku wengine wakiwa taabani kwa uchovu!

0 comments: