Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, December 30, 2011

Nilisikia nikasita kuamini. Baada ya muda habari zikasambaa mitandaoni, nikaanza kuamini. Sasa nimeamini kuwa da yangu Halima Mchuka amefariki dunia. Halima Mchuka ni dada yangu halisi kiukoo, na sote tulilijua hilo, hivyo tulielewana kama ndugu wawili . Kwa upande mwingine alikuwa mfanyakazi mwenzangu na mpendwa wote. Watu wa rika lake na marika mengine walimkubali na kumpenda. Mungu amemchukua na kazi ya Mungu haina makosa. Mungu aiweke roho ya dada halima, peponi ...amin.
Alipolazwa mara ya kwanza mara baada ya kupatwa na matatizo la kiharusi , wengi walikwenda kumjulia hali hospitalini..ikiwa ni pamoja na Raisi JK na mkewe(Pichani).

Picha ya Chini ; Halima mchuka enzi ya uhai wake..akiwa na watangazaji wenzake Kuanzia kushoto Irene Bongi, nyuma kidogo Aisha Dachi na kulia mtangazaji mkongwe Edda Sanga.

0 comments: