Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Friday, December 09, 2011

Mbwa mwenye umri mkubwa zaidi ulimwenguni kulingana na rekodi zilizopo katika kumbukumbu za ‘Guinness World Records ‘ amekufa nchini Japani akiwa na umri wa miaka 26 na miezi nane.
Mmliki wake Bi. Yumiko Shinohara aliwaambia waandishi wa habari nyumbani kwake huko Sakura , jiji lililopo nje kidogo ya Tokyo kuwa mbwa huyo aliyekuwa akiitwa Pusuke ikiwa ni mchanganyiko wa mwenye manyoya mengi laini mchanganyiko alikufa siku ya jumatatu iliyopita baada ya kuugua ghafla na kuanza kukataa kula.
Shinohara alikiambia kituo cha Televisheni cha mtandao wa FNN hapa apani kuwa anashukuru na kufarijika kwa mbwa wake kuishi kipindi kirefu hicho. Wataalamu wanasema kuwa kipindi cha kuishi mbwa kwa miaka 26 ni sawa na miaka 125 kwa binaadamu.
Kulingana na rekodi za Guinness, mbwa Pusuke huyo alizaliwa tarehe 1, mwezi April 1, 1985 na kutambuliwa kuwa ni mbwa mzee kuliko wengine mwezi desemba mwaka uliopita. Umri wa juu kabisa wa maisha ya mbwa uliwekwa na mbwa Bluey aliyeishi miaka 29 nchini Australia ambaye alikufa mwaka 1939.

0 comments: