Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Thursday, November 05, 2009


KIKAO CHA VIONGOZI WA Jumuia ya TANZANITE-JP.
Viongozi wa juu na wana kamati za Jumuiya ya watanzania wanaoishi nchini Japani (Tanzanite Society) wanatarajia kukutana Jumapili ya tarehe 8/11 katika ukumbi wa Odasaga Plaza uliopo karibu na kituo cha reli cha odakyu Sagamihara kuanzia saa 12 jioni. Baadhi ya ajenda ya kikao hiko ni kupitia na kuweka sahihi fomu za kuomba kusajiliwa kwa jumuiya kuwa NPO. Zoezi hili ambalo litasimamiwa na Mwanasheria Kijima ni hatua ya mwisho katika taratibu za usajili.Baada ya zoezi hili fomu hizi zitawasilishwa rasmi kwenye ofisi za Mkoa wa wa Tokyo.
Ajenda zingine katika mkutano huo itakuwa ni kutathmini zoezi la ulipaji wa michango ya mwezi na kuandaa ajenda za mkutano wa wanachama wote utakaofanyika tarehe 6 mwezi 12.Viongozi wote wanaombwa kufika kwenye kikao kwa wakati unaotakiwa.

Uongozi
Tanzanite Society.

0 comments: