Ni hapa...

Umefika mahali unapopahitaji ...karibu!

Posted by BM. on Saturday, February 21, 2009


Posted by BM. on Friday, February 20, 2009

Noti ya Shillingi mia enzi zake , ilikuwa na thamani kubwa sana. Mshahara wa afisa wa serikali zilikuwa noti hizo mbili miaka ya themanini. Saini zilikuwa na Cleopa David Msuya , waziri wa fedha na Charles Nyirabu , Gavana wa BOT. Upooo!

Posted by BM. on Friday, February 20, 2009

Nyumbani kwa Hayati Baba wa taifa Mwl. Julius K.Nyerere. Juu mwisho nyumba yake ya zamani.

Posted by BM. on Friday, February 20, 2009

Mzee wa Macharanga, Mtangazaji wa BBC- akitangaza kabumbu huko UK .

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Ukiwa Mwanza...na unataka kuvuka ...daladala hiyo! kandamiza moyo tu.

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Waandishi wa habari waandamizi na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari walikutana Morogoro Mwezi wa pili mwaka 2008 mjini Morogoro , kujadiliana Juu ya mwenendo wa mfuko wa BIma ya afya . Picha muhimu za kumbukumbu ya tukio hilo.
Pichani ...kufahamiana na Mhariri wa Kituo cha TV Channel 10 ni muhimu. Nyuma yetu ni paparazi Charles Hillila wa Channel 10 Kituo cha Shinyanga. Nami Nikiwakilisha TBC ....Mkoa wa Shinyanga. inapendeza.

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Meneja wa Kiss FM, Mwanza Peter Omari akimakinika katika mhadhara...Uwakilishi umetulia ...

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Aliyeketi kulia ni Daniel Msangya wa TBC kituo cha Singida , BM na aliyesimama ni Vedasto Msungu wa ITV Daima!

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Mie na Mtangazaji wa Redio Tumaini Dar ...mpiganaji mwenzangu ngoja nikupe namba!

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009


Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Bila shaka na kilaji....

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mwanza na kada mwandamizi wa CCM Mh. Stephen Mashishanga Kulia akiwa na Int. Paparazi na Komrade mwenzake hivi karibuni. Mashishanga ni miongoni mwa Viongozi nchini Tanzania aliye kipenzi kikubwa cha watu.

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Kwetu palee! Mifumo ya majitaka je!

Du!

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009


Mwanaume mmoja mwenye wivu amemuua mkewe baada ya mkewe kutaja jina la mwanaume mwingine wakati wakifanya tendo la ndoa. Colin Scully,53 amepandishwa kizimbani kwenye mahakama ya Leeds, Uingereza baada ya kumuua mkewe Tracey,39 kwa kumniga koo lake kutokana na wivu baada ya mkewe kutaja jina la mwanaume mwingine wakati wanafanya mapenzi.
Inasemekana kwamba Colin alikuwa akishuku mkewe anatoka nje ya ndoa baada ya kufanikiwa kusoma ujumbe wa simu katika simu ya mkewe lakini akaamua kufanya uchunguzi wake kimya kimya.Pamoja na jitihada zake Colin hakufanikiwa kupata ushahidi wa kuthibitisha kutoka nje kwa mkewe.Inasemekana usiku mmoja wakati wanafanya tendo la ndoa mkewe kwa bahati mbaya akamwita mumewe "Paul" jina la mwanaume mwingine.
Paul hakuwa mwingine bali ni Paul Daigton rafiki wa mkewe ambaye wako pamoja katika klabu yao ya scooter.Colin kwa hasira alimkamata mkewe shingoni na kumkandamiza kwa nguvu kwa muda mpaka alipoona mkewe hatingishiki na kumuacha na kwenda kulala chumba cha watoto wao.Inasemekana kwamba asubuhi wakati Colin akijiandaa kwenda kazini ndipo alipogundua kwamba alimuua mkewe na kuamua kupiga simu polisi "Nimemfanyia kitu mke wangu, sijui nimefanya nini".
Polisi walipofika eneo la tukio walimkamata Colin na baada ya maiti kufanyiwa uchunguzi iligundulika kwamba marehemu alifariki baada ya kukandamizwa shingoni kwa muda mrefu.Kesi yake itaendelea kusikilizwa kwenye mahakama hiyo. imekaaje hii..

Posted by BM. on Thursday, February 19, 2009

Sungusungu wa DRC; wakifanya mazoezi huko Bangadi, kaskazini mashariki mwa Kongo. Vikundi hivi vinajiandaa kupambana na majeshi ya uvamizi ya Joseph Kony ya Lord's Resistance Army. Hebu fikiria hatima ya hali hii kama haina uthibiti wa kutosha wa vikosi hivi!